Kiungo mshambuliaji Philippe Coutinho ameondoka rasmi katika klabu yake ya utotoni, Vasco da Gama, miezi sita tu baada ya kusaini mkataba wa kudumu kufuatia kipindi cha mkopo. Uamuzi huo unakuja baada ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 33 kuripotiwa kuzomewa na mashabiki wake mwenyewe katika mechi dhidi ya Volta Redonda wiki iliyopita.

Coutinho, ambaye aliwahi kung’ara katika vilabu vikubwa barani Ulaya kama Liverpool FC, FC Barcelona, FC Bayern Munich na Inter Milan, alirejea Brazil baada ya kuondoka Aston Villa. Hata hivyo, safari yake ya kurejea nyumbani imekatizwa mapema baada ya kuomba mkataba wake kuvunjwa.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kupitia ujumbe wa kihisia aliouchapisha kwenye Instagram, Coutinho alisema amechoka kisaikolojia na anaona muda wake katika klabu hiyo umefika mwisho. Alisisitiza kuwa alichagua kurejea Vasco kwa mapenzi makubwa, na kila wakati alitoa juhudi zake zote mazoezini na uwanjani.

“Nilichagua kurudi Vasco kwa sababu ninaipenda klabu hii. Kuvaa jezi hii lilikuwa moja ya maamuzi muhimu zaidi maishani mwangu. Sikuacha kujituma hata kidogo,” aliandika.
Hata hivyo, alieleza kuwa kuhukumiwa kwa mambo ambayo si sehemu ya tabia yake kumemuumiza sana, na tukio la kuzomewa lilimfanya atambue kuwa ni wakati wa kulinda afya yake ya akili. “Nimechoka sana kiakili. Si rahisi kusema haya, lakini nahitaji kuwa mkweli,” aliongeza.


