Edin Dzeko akitokea benchi mpira wake wa kwanza kugusa aliweza kuupeleka sehemu husika na kuindindikia Inter Milan goli lakwaza na kufanya ubao usomeke 1-1.
Dzeko aliyeingia kipindi cha pili akichukua nafasi ya Joaquin Correa dakika ya 57, na ndani ya dakika moja tu alipokea pasi kutoka kwa Ivan Perisic na kufunga goli safi na kufanya ubao usomeke 1-1.

Mshambuliaji huyo kutokea Bosnia pia alisababisha penati baada ya golikipa Andrea Consigli kumchezea madhambi kwenye eneo la hatari ndani ya boksi mwamuzi kuwazawadia penati ma Lautaro Martinez kubadilisha ubao na na kusomeka 2-1.
Edin Dzeko alisema, “nimefunga magoli mengi lakini sikumbuki kama nishafunga kwenye mpira wangu wa kwanza kugusa, kila kitu kina mwanzo, najua ni kiasi natakiwa kujitoa, Inter wanajua hilo pia ndio maana wakanisajiri.”
Inter wamepanda mapaka nafasi ya pili wakiwa na pointi 17, pointi moja nyuma ya vinara Napoli, ambao wamesafili kwenda fiorentina kucheza na Sassuolo ambao wako nafasi ya 13 wakiwa na pointi 7.
Ushindi wa Inter Milan unawapa uwiano wa ushindi wa goli mbili kwenye michezo 12 ya ligi mfululizo, wakipindua ushindi mrefu zaidi wa kushinda michezo 11 mwaka 1943.
SPACE SPIN NA MERIDIANBET.
Ni Mabingwa pekee Meridianbet wanakupa nafasi ya kushinda zaidi na mchezo wa Space Spin katika kasino bomba za meridianbet. Ni wakati wa kufurahia na kutengeza mkwanja bila kuwaza.


