Kwa umbo na umri ni kijana mdogo tu (miaka 21) lakini, uwezo wake kwenye safu ya ulinzi ni mkubwa sana. Huyu ni Wesley Fofana.
Fofana amekuwa ni pengo kwenye safu ya ulinzi ya Leicester City msimu huu. Hii ni kutokana na kupata majeraha wakati wa maandalizi ya msimu huu na toka hapo, hajarejea tena uwanjani kuitumikia timu hiyo msimu huu.

Kwa msimu wa 2020/21, Wesley aliitumikia The Foxes kwenye jumla ya michezo 38 ukiwa ndio msimu wake wa kwanza na klabu hiyo.
https://twitter.com/LCFC/status/1500863855496339456?s=20&t=L_uM1GmPvFCHbyz2eJxPsA
Licha ya kuwa nje ya uwanja, Fofana ameongeza mkataba wa miaka 5 kuendelea kubaki King Power Stadium. Kwa maana hiyo, beki huyu ataendelea kuitumikia Leicester City mpaka 2027.
Kwa hali ilivyo, huenda Wesley akarejea uwanjani wiki hii wakati ambapo, Leicester City watachuana na Rennes kwenye mchezo wa Ligi ya Europa.
Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000 katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.


