Mwanariadha machachari Usain Bolt kwa sasa anafurahia kuanza kazi yake katika soka. Mwanariadha huyu ambae kwa mujibu wa Jarida la Forbes Juni 2017 ana utajiri unaokadiriwa kuwa na thamani ya dola za kimarekani milioni 34.2 akiwa kwenye orodha ya wanariadha wanaolipwa zaidi duniani.
Bolt amekuwa akifanya mazoezi ya soka na kwa sasa yupo na upande wa Australia Central Coast Mariners. Mwanariadha huyu anatamani kuja kuichezea club ya Man Utd japokuwa duru zinahoji kama mwanariadha huyu anaviwango stahiki kuingia Man Utd?.
Bolt amesherekea siku yake ya kuzaliwa jana tarehe 21 Agust akiwa anatimiza umri wa miaka 32 alisisitiza nia yake ya kuhamia kwenye soka huku akidai huu ni wakati wake muafaka wa kujifunza na kuwa mchezaji wa kulipwa na atajifunza na kuwa bora zaidi kufikia levo hizo.
Uwezo wa Bolt katika soka unatiliwa shaka na baadhi ya wanasoka ambao wamebahatika kumuona akijifunza na kucheza lakini baadhi wanaamini atafikia mafanikio fulani lakini kwa kuongeza nguvu kubwa sana na jitihada za ziada.



Nasra
Wamsaini tu
Fatina mfingi
Makal nzur
Povel
Habar njema