Kinda wa Chelsea Billy Gilmour mwenye miaka 17 anasema anataka kuwa mchezaji bora zaidi Duniani. Gilmour alijiunga na Chelsea akiwa na miaka 16 mwaka 2017 kwenye kikosi cha vijana wa chini ya miaka 18, mwezi Julai 2018 amejiunga na kikosi cha vijana wa chini ya miaka 23.
Gilmour ameanza kung’ara katika midani za kimataifa anatazamiwa kuja kuwa mchezaji mkubwa sana baadae. Nafasi yake uwanjani ni kiungo, akiwa na timu ya vijana wenye umri chini ya miaka 18 amefunga magoli 8 katika gemu 21 alizocheza. Kikosi cha vijana wenye umri wa miaka chini ya 23 amefunga goli mara moja na kutoa pasi 2 za magoli.
Kinda huyu alizungumza na chanzo cha habari Daily Mail akasema “Hii ndio hamu yangu ya wakati wote, kuwa bora duniani, kama kuna mtu ni bora zaidi yangu mimi nataka kuwa bora zaidi yao! nachukia sana kushindwa na mda wote nimekuwa nikifikiria ushinndi.” anasisitiza yuko tayari kufanya jitihada ili aweze kuiishi ndoto yake hiyo ya kuwa mwansoka bora duniani.


Povel
Dogo yupo vzr sana
Furahav
Pambana utimize ndoto zako.