City Kutumia Paundi 350M Usajili

Timu zimeanza kuweka mezani mipango ya kutumia pesa nyingi kuwabamba wachezaji wakali msimu huu unakuja wa joto. Manchester City kama klabu zingine nao kama kawaida wapo kwenye mpango wa kukipa nguvu zaidi kikosi kwa fungu la paundi 350m wakati wa usajili.

Kwa mujibu wa ripoti meneja Pep Guardiola anapanga kutumia kitita hicho cha pesa kuwanasa wachezaji wanne watakaoongeza moto klabuni hapo wakilenga beki wa kushoto na kiungo pia.

Mancity ambao kwa sasa wanafukuzia mataji manne kuelekea mwisho wa msimu wanasaka kuwa na kikosi bora zaidi kwenye Ligi Kuu ya Uingereza. “kuna nafasi tatu au nne hivi natakiwa kuziangazia lakini pia kuna mawazo ambayo tunayo” -Guardiola

Guardiola anadaiwa kuwa anamuangazia nyota wa Leicester Ben Chilwell baada ya kuona kuwa hataweza kumuamini Benjamini Mendy ambaye anaonekana kama hajakuwa na matokeo yale wanayoyategemea. Guardiola anafikiria mastaa wengine watakaoingia kwenye orodha ya kutumia kitita hicho.

4 Komentara

    Wasajili tu jamani tupate raha #Meridianbettz

    Jibu

    Pesa inaongea

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.