Ripoti za kina zinasema kuwa kipigo kichungu cha Intermilan alichokipokea kwenye Dabi d’Italia wikendi kimesababisha mashaka yanayomzunguka kocha Simone Inzaghi kuibuka tena.

Inter walipata kichapo kibaya cha mabao 2-0 kutoka kwa wapinzani wao Juventus wikendi, matokeo ambayo yanawaacha nafasi ya 7 kwenye msimamo wa Ligi Serie A wakiwa nyuma pointi 11 dhidi ya vinara Napoli.
Inter wamekatishwa tamaa katika migongano ya moja kwa moja na timu za juu, wakipoteza dhidi ya Juventus, Roma, Milan na Lazio, na urefu wa Ligi ya Mabingwa mwezi uliopita unaonekana kuwa mbali sasa.
Kama ilivyoripotiwa na La Gazzetta dello Sport na Corriere della Sera, wasimamizi wa Inter wanaweza kukutana ana kwa ana na Inzaghi kabla ya mechi ya Inter dhidi ya Bologna kesho, wakitaka kumkumbusha kwamba kumaliza nafasi ya nne ni lazima msimu huu.
Nerazzurri hawawezi kumudu kupoteza pesa muhimu za Ligi ya Mabingwa na presha inazidi kupanda kwa Inzaghi, ambaye anahitaji kuanza kuiongoza klabu hiyo kwenye msimamo haraka baada ya mapumziko ya Kombe la Dunia.
Ulishawahi kuwaza kuwa rubani wa maisha yako!! Kuwa rubani wa mchezo pendwa wa Aviator wa kasino mtandaoni. Aviator bonanza inazidi kutoa michongo ya mkwanja kwenye nyumba ya mabingwa. Unarusha ndege yako na unashinda, kuwa rubani wa kujivunia kwa kuibuka na mkwanja leo.
BONYEZA HAPA