Inter imepoteza mechi yake ya kwanza ya msimu huu usiku wa jana baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Udinese waliocheza kwa ari kubwa na kugeuza matokeo kutoka nyuma, na kuishtua timu ya Cristian Chivu huku Thuram akisema kuwa hawakustahili.

Akizungumza na Inter TV baada ya mchezo (kupitia FCInterNews), mshambuliaji wa Nerazzurri, Marcus Thuram, alionekana mtulivu akisema, “Hatuwezi kukata tamaa, tulizungumza vizuri ndani ya chumba cha kubadilishia nguo.”
Thuram alikubali kuwa wao kama timu walijua mechi hiyo ingekuwa ngumu, baada ya kuona Udinese wakionyesha ubora dhidi ya finalisti wa Ligi ya Mabingwa msimu uliopita, “Tulijua ingekuwa mechi ngumu. Katika msimu kuna michezo migumu kama hii.”
Leo hii unaweza kutusua mkwanja mrefu endapo utacheza michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile Aviator, Poker, Roullette, Keno, Super Heli na mingine kibao. Ingia Meridianbet sasa na ucheze hapa.
Mfaransa huyo alitoa pasi ya bao kwa Denzel Dumfries aliyefunga bao la kwanza, kabla ya Udinese kufunga magoli mawili ya kushtukiza na kuiacha San Siro ikiwa kimya kwa mara ya pili ndani ya wiki moja baada ya wapinzani wao wakubwa, AC Milan, kufungwa mechi ya ufunguzi na Cremonese ya Davide Nicola.


