Liverpool wameamua kujitoa katika kumfukuzia kiungo Mfaransa Adrien Rabiot na kuwaacha Juventus, Milan na Barcelona wakimfukuzia staa huyo kutoka Paris-Saint Germain.
Staa huyu mfaranca, mwenye miaka 23 amechomoa kusaini mkataba mpya huku makataba wake ukiwa unaisha mwezi Juni 2019 na baada ya hapo atakuwa huru kujiunga na klabu yeyote. Kama PSG watahitaji kutompoteza bure staa huyu watalazimika kumuuza mapema mwezi Januari. Kadri mkataba wake unavyokaribia mwisho ndivyo thamani yake inavyozidi kupungua hivyo bado hawatakuwa na dau kubwa sana la kumuuza mchezaji huyu.
Juventus, Milan na Barcelona bado wanasisitiza nia zao za kumnasa mkali huyu, kwa msimu huu Rabiot amefunga goli moja na kutoa pasi 5 za usaidizi akiwa na PSG.



Fatina
Asanteh kwa taarifa meridian
isha
Makala nzuri
Sadick
Hatimae Juventus alichukua mwali#meridianbettz
Povel tz
Duh kila la kheri