Golia wa Man City Claudio Bravo amepata jeraha kwenye mguu akiwa mazoezini jumatatu ambalo limekuwa kikwazo kwa timu hiyo kutokana na umuhimu wake. Golia huyo mwenye umri wa miaka 35 amethibitishwa kuwa atasafiri kuelekea Barcelona kwa ajili ya vipimo zaidi.
Jeraha la Claudio Bravo linawaacha man city wakiwa tegemezi kwa Daniel Grimshaw mwenye umri wa miaka 20 kama mbadala wa chaguo la kwanza bwana Ederson Wakati huo Midfielder Kevin de Bruyne tayari yuko nje kwa mda wa miezi mitatu kwa ajili ya tatizo alilopata kwenye goti lake.
Bwana Bravco alisaini kuichezea timu hiyo akiwa anatokea Barcelona kwa ada ya Euro milion 15.4 mwaka 2016 na kumfanya meneja Pep Guardiola kuwa na tegemeo la uhakika.
Uwepo wa Claudio Bravo katika Man city ulimfanya Pep Guardiola Kuwauza golia muingereza bwana Angus Gunn mwenye umri wa miaka 21 kwenda Southampton mwezi julai na Joe Hart kwenda Burnley mwezi August.

