Meneja wa West Ham, Manuel Pellegrini ameweka wazi mipango yake kwa msimu unaofuata akisisitiza klabu yake kumaliza katika sita bora kwenye Ligi Kuu ya Uingereza msimu ujao.
Meneja huyu ambaye pia amewahi kuwa meneja wa Manchester City, anadaiwa kuwa ameleta utulive katika dimba la London kwenye msimu nwake wa kwanza na klabu ya West Ham wakiwa wamefanikiwa kuwepo kwenye 10 bora kipindi hiki wakisalia na gemu 10 za mwisho kwenye msimamo wa ligi.
Meneja huyu anadaiwa kuwa amerejesha hali ya kujiamini klabunia hapo, huku akiongeza kandarasi mpya za wachezaji ambao wameongeza nguyvu klabuni hapo kama Filipe Anderson na vijana kama Declan Rice wanaotokea Academy ya klabu hiyo.
Meneja huyu akitambua kuwa bado wana kibarua kikubwa msimu huu anassema “Tunashindwa kutazama msimu ujao kwa sasa kwa sababu bado tunahitaji kumaliza msdimu huu.”
“hatua inayofuata ni kujaribu kusajili wachezaji vijana wengi zaidi ili tuendelee kuwa na kikosi kizuri zaidi cha vijana na kujaribu kufikia sita bora kwenye Ligi Kuu.
Pellegrini naamini anahitaji wachezaji wengi vijana klabun i hapo ili aweze kutoboa kufikia angalau nafasi ya sita. Akitaja changamoto kubwa kwenye usajili anasema klabu nyingi kubwa zinatumia pesa zake kusajili wachezaji wazuri hivyo wanashindwa kupata wachezaji kwa sababu hawana pesa. Hata hivyo anaamini kusajili vijana inaweza kuwa suluhisho.


Mariam mtandama
Asante kwa taarifa
Caroline
Asante meridian bet Kwa update
Furahav
Habari nzuri.
Zeiyana
Habari nzuri sana
Fatina mfingi
Ni habar njema