Rulani Mokwena anaendelea kuonyesha kwa vitendo kuwa safari yake Algeria si ya majaribio bali ya kutengeneza historia. Kocha huyo wa Afrika Kusini ameiongoza MC Alger kuvuka hatua nyingine muhimu kwenye Kombe la Algeria, ushindi ambao unaongeza imani na uzito wa mradi anaoujenga ndani ya klabu hiyo kongwe ya Afrika Kaskazini.
Katika mchezo wa hatua ya 16 bora dhidi ya Ben Aknoun, MC Alger ilifanikiwa kuondoka na ushindi wa 1-0. Licha ya kutawala umiliki wa mpira na kucheza zaidi katika nusu ya mpinzani wao kwa dakika 90, safu ya ushambuliaji ya MCA ilikosa umakini, na kufanya mchezo uende hadi dakika za nyongeza bila mshindi kupatikana.
Mwokozi wa mchezo alikuwa ni winga raia wa Ivory Coast, Kipre Zunon, aliyefunga bao la pekee dakika ya 96. Bao hilo halikuwa tu tiketi ya kufuzu robo fainali, bali pia lilidhihirisha kina cha kikosi cha Mokwena na uwezo wake wa kupata suluhisho hata pale mpango wa awali unapokutana na changamoto.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa sasa, macho ya MC Alger yanaelekezwa kwenye robo fainali, ambapo watakutana na mshindi kati ya CS Constantine na ES Setif. Mchezo huo una mvuto wa kipekee kutokana na uwepo wa kocha Milutin “Micho” Sredojevic wa ES Setif, jina linalofahamika sana katika soka la Afrika.



