Folz Afichua Sababu Kufukuzwa Yanga, Haikua Matokeo

Kocha wa zamani wa Young Africans, Romain Folz, amefunguka kuhusu kuachishwa kwake kazi na Young Africans SC, akieleza kuwa uamuzi huo ulikuwa ni matokeo ya mambo yasiyo na maana. Folz, ambaye pia amefundisha timu za AmaZulu na Marumo Gallants, na pia kocha msaidizi wa Mamelod Sundowns, zote za nchini Afrika Kusini, aliungana na Yanga mnamo Julai 2025 kwa lengo la kuendeleza mafanikio ya klabu nchini na kuifanya ionekane kwenye mashindano ya kimataifa ya Afrika. 

Hata hivyo, safari yake nchini Tanzania ilikatizwa baada ya miezi mitatu tu, huku ripoti zikieleza kuwa kuondoka kwake kulihusiana na kipigo cha 1-0 kilichopokelewa na timu yake dhidi ya Silver Strikers katika mechi ya kwanza ya hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika Oktoba mwaka jana.

Folz Afichua Sababu Kufukuzwa Yanga, Haikua Matokeo

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Folz ambaye alishinda taji moja na Yanga, alisisitiza kuwa kuachishwa kwake hakuhusiani na utendaji wa timu uwanjani, bali ni matatizo ya ndani ya klabu aliyoyaona hayakubaliki. “Matokeo yalikuwa mazuri, na timu ilikuwa ikiboreshwa vizuri sana kimfumo. Kushinda taji la Ngao ya jamii lilikuwa ni jambo zuri kabisa,” alisema.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Kocha huyo aliongeza kuwa mzozo huo wa ndani ulikuwa ni changamoto, na kufanya kazi yake kuwa ngumu. “Mimi nafanya kazi kushinda, hivyo ni furaha kubwa kushinda taji. Kuachishwa kwangu kulitokana na mzunguko mkubwa wa mambo yasiyo na maana ambayo wafanyakazi wangu walipaswa kuyashughulikia. Hili siyo jambo ambalo ninaweza kulivumilia. Niliondolewa baada ya kupoteza mechi yangu ya kwanza tu, baada ya kufungwa bao moja pekee. Hiyo haikuwa kosa langu wala la wafanyakazi wangu,” alisema Folz.

Folz Afichua Sababu Kufukuzwa Yanga, Haikua Matokeo

Aidha, Folz alionyesha kuwa timu ingekuwa na matokeo bora zaidi kama matatizo haya ya ndani yasingekuwepo. “Maandalizi yetu yalivurugika sana kwa matatizo ya ndani, na nilipinga vikali hili. Bila hayo, naweza kudhibitisha kuwa tungekuwa hatupotezi mechi yoyote. Nilifanya sehemu yangu na nikaleta taji. Licha ya yote, lazima niendelee kufanya kazi kitaalamu.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.