Leo jioni, macho na masikio ya mashabiki wa soka nchini yataelekezwa Pemba ambako uwanja wa Gombani unatarajiwa kuwa jukwaa la maamuzi. Kuanzia saa 10:30 jioni, Yanga na Azam FC zitapambana uso kwa uso katika fainali ya Kombe la Mapinduzi, mechi inayobeba uzito wa heshima, historia na fahari ya klabu.
Yanga wamefika hatua hii baada ya safari ngumu waliyoipitia kuanzia hatua ya makundi mpaka sasa fainali. Katika hatua ya nusu fainali, waliwaondoa Singida Black Stars kwa ushindi mwembamba wa bao 1-0, matokeo yaliyoonesha uimara wa klabu hiyo.
Kwa upande wa Azam FC, safari yao haikuwa rahisi hata kidogo. Walilazimika kupambana vikali dhidi ya Simba SC katika nusu fainali, lakini kwa umakini na mpango mzuri wa kiufundi, waliibuka na ushindi wa 1-0. Matokeo hayo yamewapa Azam ujasiri mkubwa wanapoingia kwenye fainali hii ya maamuzi.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Fainali ya leo haitakuwa tu kuhusu vipaji uwanjani, bali pia mbinu za makocha na uwezo wa wachezaji kustahimili presha. Yanga wataingia wakiwa na hamasa ya kuthibitisha ubora wao, huku Azam FC wakisaka taji ili kuonesha kuwa wao ni nguvu inayopaswa kuhofiwa katika soka la Tanzania.
Kadri saa zinavyosogea kuelekea filimbi ya kwanza, swali moja linatawala vichwa vya mashabiki, ni nani atakayenyanyua Kombe la Mapinduzi leo? Je, itakuwa ni Young Africans au Azam FC? Majibu yote yatapatikana Pemba, ndani ya dakika 90 za burudani ya soka.