Azam FC imeendelea kuonyesha dhamira yake ya kurejesha makali ya ushindani kwa kufanya usajili wa kimkakati wa mshambuliaji Aimar Hafidh Abubakar maarufu kama “Haaland”, akitokea klabu ya Mlandege ya Zanzibar.
Aimar amejijengea jina lake akiwa Zanzibar kutokana na uwezo wake wa kucheza kama mshambuliaji wa kisasa anayejua kutafuta nafasi, kutumia nguvu ya mwili na kumalizia mashambulizi kwa ufanisi. Akiwa na Mlandege, amekuwa miongoni mwa wachezaji waliovutia macho ya wengi kutokana, kasi, na uwezo wa kucheza ndani ya boksi.

Kupitia taarifa rasmi, Azam FC imeeleza kuwa imeridhishwa na ufundi wa mchezaji huyo, akitajwa kuendana na falsafa ya soka ya klabu inayojikita katika umiliki wa mpira na kasi ya kushambulia. Uzoefu wa Aimar katika ligi za ndani, pamoja na mazoea ya ushindani mkali Zanzibar, vinatajwa kuwa faida muhimu atakazokuja nazo Chamazi.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa Azam FC, usajili huu unakuja wakati muafaka ambapo klabu inalenga kuboresha rekodi yake ya ufungaji mabao baada ya misimu iliyopita kuonyesha hitaji la mshambuliaji mwenye makali. Uwepo wa Aimar unatarajiwa kuongeza chaguo kwa benchi la ufundi, kutoa ushindani wa nafasi, na kusaidia timu kupata matokeo chanya katika ratiba ngumu ya timu hii.

Sasa macho yote yanaelekezwa uwanjani, ambako mashabiki wa Azam FC wanasubiri kuona kama “Haaland” wa Zanzibar ataweza kuthibitisha jina lake kwa vitendo akiwa na jezi ya rangi nyeupe na bluu.


