Wayne Rooney amewaambia wachezaji nyota wa Manchester United inabidi wathibitishe na kuonesha wanajari kama Ole Gunnar Solskjaer anavyopambana kuweza kuokoa kibarua chake.
Nyota huyo wa zamani wa Man Utd alisema, “kupokea kipigo cha goli 5-0 dhidi ya mahasimu Liverpool jumapili, sio rahisi kuangalia tena ule mchezo, Man Utd wamedhalilishwa sana.”

“Wachezaji inabidi wajiulize wao wenyewe, ni sawa kocha kubeba lawama zote wakati wachezaji wanalipwa pesa nyingi kwa ajiri ya kufanya hiyo kazi na hawafanyi ipasavyo.”
“Hilo ni jukunu la wachezaji wote, wachezaji wa kiwango cha Dunia na kimataifa na klabu kama Man Utd inahitaji zaidi, wacheaji inabidi waumie wanapopoteza mchezo.”
“Najua Ole anapambana, na ataendelea kufanya kitu sahihi, na ataendelea kuamini kile anachokiamini na tajaribu zaidi na zaidi kupata zaidi kutoka kwa wachezaji sababu ni jukumu lao.”
Manchester United kesho anakutana na Tottenham kwenye mchezo wa ligi kuu ya Uingereza huku Man Utd akiwa na kumbukumbu ya kupoteza kwa goli tano bila dhidi ya Liverpool wikiendi iliyopita.
Mchongo wa mkwanja mrefu kutoka kasino bora za mtandaoni za Meridianbet. Mchezo wa Circus Fever unakuweka katika nafasi nzuri ya kuwa mshindi. Furahia kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa meridianbettz.

CHEZA HAPA

