Ancelotti: Sihofii Kuhusu Mikataba ya Asensio na Ceballos

Kocha wa klabu ya Real Madrid Carlo Ancelotti amesema yeye hana hofu kuhusu mikataba ya wachezaji wake wawili Marco Asensio pamoja na Dani Ceballos.

Kocha huyo amezungumza juu ya wachezaji wake hao ambao mikataba yao inamalizika hivi karibuni baada ya kusema mazungumzo yanaendelea juu ya wachezaji hao, Huku akisema atakua na furaha kama wachezaji hao watasalia lakini hivohivo kama wataamua kuondoka.ancelottiWachezaji hao wawili Marco Asensio na Dani Ceballos wanakaribia kumaliza mikataba yao ndani ya klabu hiyo mabingwa watetezi wa ligi ya mabingwa barani ulaya, Wachezaji hao kwasasa wanafanya mazungumzo na klabu hiyo na kama mambo yataenda vizuri basi watasalia klabuni hapo.

Carlo Ancelotti pia amezungumza kuhusu mchezaji wake Eden Hazard ambaye hajakua na msimu mzuri, Lakini kocha huyo amewatoa hofu mashabiki kwa kusema Hazard yuko vizuri anafanya vizuri mazoezini na yupo tayari kwa mzunguko wa pili wa msimu.ancelottiKocha Ancelotti ambaye nae ameongeza mkataba klabuni hapo msimu huu utakaombakiza ndani ya Real Madrid mpaka 2024, anatarajiwa kuiongoza timu hiyo leo kuelekea mchezo wao dhidi ya klabu ya Real Valladolid wakiwa ugenini.

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.