Barcelona Yabanwa Mbavu

Klabu ya Fc Barcelona imeshindwa kupata alama tatu muhimu kwenye mchezo wa Derby ya jiji hilo dhidi ya klabu ya Espanyol baada ya kulazimishwa sare ya goli moja kwa moja.

Wababe hao wa Catalans walifanikiwa kupata bao mapema kabisa kwenye kipindi cha kwanza kupitia kwa beki wa kushoto Marcos Alonso, Na kufanikiwa kuwapa Barca uongozi mpaka mchezo unaenda mapumziko klabu hiyo ilikua mbele kwa bao moja.barcelonaKipindi cha pili kiliendelea huku klabu ya Barcelona ikionekana kuhitaji bao la pili kutokana na kulisakama lango la Espanyol ka kiwango kikubwa, Lakini klabu ya Espanyol walionekana kua watulivu na kuzuia kwa nidhamu ya hali ya juu.

Klabu ya Espanyol walifanikiwa kufanya shambulizi la hatari kwenye lango la Barca mpaka kupelekea kupata mkwaju wa penati na kuwekwa kimiani na Joselu dakika ya 73 ya mchezo, Na kuufanya mchezo kua sare mpaka dakika ya tisini ya mchezo.barcelonaKlabu ya Barcelona imeendelea kusalia kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya La liga kwa tofauti ya magoli, Kwani wanalingana alama na klabu ya Real Madrid wakiwa na alama 38 kila mmoja baada ya Real Madrid kudhinda mchezo wa jana.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.