Griezmann Haondoki Atletico Madrid

Mshambuliaji wa klabu ya Atletico Madrid na timu ya taifa ya Ufaransa Antoine Griezmann inaelezwa hana mpango wa kutimka ndani ya klabu hiyo baada ya kuhusishwa na kujiunga na Man United.

Antoine Griezmann siku kadhaa nyuma amekua akihusishwa na kujiunga na klabu ya Manchester United, Lakini vyanzo vya ndani kutoka klabu ya Atletico Madrid vinaeleza staa huyo hana mpango wa kutimka klabuni hapo.griezmannInafahamika kua mshambuliaji huyo amewekeza akili yake ndani ya viunga vya Wanda Metropolitano baada ya kukataa ofa ya kujiunga klabu mbalimbali za Saudia, Hivo suala la yeye kujiunga na Man United ni jambo ambalo sio rahisi.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa amekua kwenye kiwango kizuri sana msimu ndani ya Atletico Madrid, Jambo ambalo limewafanya klabu ya Manchester United kufukuzia saini ya mchezaji huyo.griezmannAntoine Griezmann ni wazi hana mpango wa kuondoka ndani ya klabu ya hiyo na kutimkia timu yeyote, Kwani kama ni kuondoka angeondoka dirisha kubwa lililopita ambapo alipewa ofa kubwa na vilabu kutoka nchini Saudia Arabia.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.