Fulham wameripotiwa kuifahamisha Liverpool kwamba kinda Fabio Carvalho anayehitajika Liverpool hauzwi kwenye dirisha la usajili la Januari.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 amekuwa kwenye fomu nzuri akiwa na Cottagers kwenye kampeni ya 2021-22, akifunga mara saba na kuchangia mabao manne katika mechi 19 katika mashindano yote.
Mkataba wa Carvalho katika klabu ya Craven Cottage unatarajiwa kuisha msimu huu wa joto, na Liverpool ni miongoni mwa vilabu vinavyotajwa kuhitaji huduma ya mshambuliaji huyo.

Kwa mujibu wa gazeti la The Sun, Liverpool hivi majuzi waliwasiliana na klabu hiyo kufahamu kuhusu upatikanaji wa kijana huyo lakini waliambiwa kwamba hauzwi kwenye dirisha la januari.
Ripoti hiyo inadai kwamba Fulham wanatamani sana Carvalho kusaidia harakati zao za kupanda Ligi Kuu na kwa hivyo watakataa ofa zozote zitakazowasili mwezi huu.
Kinda huyo anahusishwa na Chelsea, Real Madrid na West Ham United. Staa huyu amefunga mabao nane na kusajili mabao manne katika mechi 25 alizoichezea Fulham tangu aingie kwenye kikosi cha kwanza.
Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.


