Tetesi za Soka Barani Ulaya.

 

Tetesi zinasema, mshambuliaji wa Borussia Dortmund, Erling Braut Haaland, 21, anataka kusubiri kuchukua uamuzi ili kuona iwapo Barcelona wataweza kumsajili.

Tetesi zinasema, West Ham United imetoa dau la pauni milioni 50 kwa ajili ya kiungo wa kati wa Leeds United na England Kalvin Phillips mwenye umri wa miaka 26.

Manchester City watasikiliza ofa kwaajili ya mshambuliaji wa England Raheem Sterling, 27 msimu huu kama watashindwa kukubaliana naye juu ya kurefushwa kwa mkataba wake ambao utaisha msimu wa kiangazi wa mwaka 2023.

 

Barcelona Yamtaka Sterling Nou Camp.

Barcelona wamefikia makubaliano na mshambuliaji wa Gabon mwenye umri wa miaka 32 Pierre-Emerick Aubameyang kwa mkopo kutoka Arsenal lakini watahitaji kumuachilia Dembele ili kukamilisha taratibu za uhamisho.

Tetesi zinasema, Everton imejiunga na Crystal Palace katika kinyang’anyiro cha kumsaijili kiungo wa kati wa Uholanzi, Donny van de Beek, 24 kwa mkopo kutoka Manchester United.

Tetesi zinasema, Tottenham wametoa ofa ya Euro milioni 30 na marupurupu ya ziada kiungo wa kati wa Juventus Rodrigo Bentancur, ambaye pia anawaniwa na Aston Villa.

 

Saliba Ajiandaa Kurejea Nice kwa Mkopo.

 

Mlinzi wa Arsenal mwenye umri wa miaka 20- Mfaransa William Saliba, ambaye anacheza kwa mkopo katika Marseille, yuko katika orodha ya wachezaji wanaolengwa na Real Madrid msimu huu.

Tetesi zinasema, Arsenal wamekataa dau la pili kutoka kwa Crystal Palace kwa ajili ya mshambuliaji Muingereza Eddie Nketiah, ambaye mkataba wake unaisha msimu huu.

Newcastle imeongeza dao la pauni milioni £10m na zaidi kwaajili ya mlinzi Muingereza Dan Burn, 29, lakini Brighton ilikataa, inataka kati ya pauni milioni 12 na milioni 15.


VUNA MKWANJA NA KENO

Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.

tetesi, Tetesi za Soka barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe