Giovanni van Bronckhorst Kutua Rangers.

 

Kocha msaidizi wa timu ya Taifa ya Uholanzi, Giovanni van Bronckhorst anatarajiwa kuchukua mikoba ya kuinoa klabu ya Rangers baada ya kufikia makubaliano ya uongozi wa klabu hiyo.

 

Giovanni van Bronckhorst ambaye pia amewahi kukitumikia kikosi cha Rangers (1998-2001) anarudi tena Ibrox kuchukua mikoba ilioachwa na Steven Gerrard aliyejiunga na klabu ya Aston Villa.

Van Bronckhorst alionekana London siku ya jumamosi ambapo inasemekana alifanya mazungumzo chanya na uongozi wa Klabu ya Rangers kabla ya kurejea Uholanzi.

Van Bronckhorst alijiunga na Arsenal na kufanikiwa kuchukua ubingwa wa ligi kuu, kabla ya baadae kujiunga na Barcelona na hatimae Feyenoord.

Rangers wanaongoza kwa alama 4 mbele ya Celtic katika msimamo wa ligi ya Scotland baada ya michezo 13. Mechi inayofuata itakua dhidi ya Hibernian kwenye nusu fainali ya kombe la ligi pale Hampden Park.


WIKI NJEMA NA CRAZY TIME CASINO!

Unasababu milioni za kucheza unavyotaka ukiwa na mabingwa meridianbet, lakini unasababu moja ya kushinda mamilioni katika kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo maridhawa wa Crazy Time unakupa sababu hizo kuwa mmoja wa washindi leo hii.

 

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe