Griezmann Atakuwa Msaada Mkubwa Barcelona -Koeman.


Kocha Ronald Koeman amesema fowadi Antoine Griezmann ndiye atasalia mwanasoka nguzo atakayetegemewa na Barcelona kadri kikosi hicho kinachojiandaa upya kwaajili ya msimu ujao.

Barcelona tayari wamefichua azma ya kuagana rasmi na mshambuliaji Luis Suarez huku wakitazamiwa pia kukatiza uhusiano na nahodha Lionel Messi anayehusishwa pakubwa na Manchester City, PSG na Inter Milan.

Suarez kwa upande wake anawaniwa pakubwa na Juventus na Atletico Madrid.

 

Griezmann Atakuwa Msaada Mkubwa Barcelona -Koeman.

Kwa mujibu wa wakala Eric Olhats, Griezmann alikuwa tayari kuondoka Camp Nou mwishoni mwa msimu huu baada ya kulazimika kucheza katika nafasi ambayo hajaizoea kila mara alipowajibishwa kwa pamoja na Messi na Suarez katika klabu ya Barcelona.

“Alishiriki kikao na Koeman ambaye kwa sasa amemhakikishia kwamba atamchezesha katika nafasi inayomfaa zaidi uwanjani,” akasema Olhats.

Griezmann ambaye ni mzawa wa Ufaransa, alisajiliwa na Barcelona kutoka Atletico kwa kima cha Sh14 bilioni mwanzoni mwa msimu huu wa 2019-20.

Hata hivyo, hakuridhisha jinsi ilivyotarajiwa huku akichezeshwa kwa dakika zote 90 za mechi moja mara 19 pekee.

Chini ya wakufunzi Ernesto Valverde na Quique Setien waliopigwa kalamu na Barcelona msimu huu, Griezmann alifunga mabao 15 pekee kutokana na mechi 48.

 

Griezmann Atakuwa Msaada Mkubwa Barcelona -Koeman.

“Alikuwa amefikia maamuzi ya kuagana na Barcelona hata kabla ya mechi ya robo-fainali ya UEFA iliyowashuhudia wakipigwa 8-2 na Bayern Munich.

Dalili zote ziliashiria kwamba hakuwa sehemu ya mipango ya klabu na hakuwa katika mawazo ya kocha. Hata hivyo, kwa sasa yuko radhi kusalia Camp Nou na Koeman atamuunga mkono kwa mengi,” akaongeza Olhats.

Kwa mujibu wa gazeti la L’Equipe, Griezmann kwa sasa atavaa jezi namba saba mgongoni badala ya 17 msimu ujao.

“Kwa heshima zote, Griezmann lazima arejee kucheza katika nafasi aliyozoea kutoka kwa waajiri wake wa zamani na timu ya taifa. Hapa ndipo msaada na ushauri wa kocha unahitajika zaidi,” akasema Koeman.


SHINDA NA HI LO

Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.

Cheza Sasa.

44 Komentara

    Good news 👍
    @meridianbettz

    Jibu

    Ni habari njema sana pale barca watakapo kuwa na luis suarez lkn inatupa mashaka kidogo Messi atakapotoka cjui kikosi kitakuaje#Meridianbettz

    Jibu

    Hatimaye griezman anarejea Barcelona imekaa poa sana hii 👍

    Jibu

    griezmann ni mahili sana katika mpira na atafanya mambo makubwa sana barcelona

    Jibu

    Koeman kaongea ukweli

    Jibu

    Hilo ndio tumaini lingine Barca alilobaki nalo ukimtoa Messi ataisaidia timu vizuri tu

    Jibu

    Griezmann anakuja kuziba pengo la mess

    Jibu

    Ni wakati wa Griezmann kuonyesha balaa lake sasa akiwa na Koeman

    Jibu

    Hatimaye griezman anarejea barcelona

    Jibu

    habar njema

    Jibu

    hawa Barcelona wamekua kama wafa maji wanatapatapa tu

    Jibu

    Barcelona iko poa sana

    Jibu

    Arejea Barcelona na kuleta mafanikio makubwa.

    Jibu

    Griezmann anataka kuonesha mahajabu yake yupo vizuri

    Jibu

    Barcelona timu kubwa

    Jibu

    Jambo zuri

    Jibu

    sawa ndo chaguo la kocha

    Jibu

    Habar njema

    Jibu

    Barcelona ndio wajipange sasa

    Jibu

    Sasa wajipange vizuri msimu huu ili wasirudi nyuma tena#meridianbett

    Jibu

    Good news 👍

    Jibu

    Koeman yuko sahii.

    Jibu

    Ni kwer endapo mess atasep tutamuon grezman wa Atletico mweny njaa ya magor

    Jibu

    Barcelon chama la wana

    Jibu

    Safi sana anaweza kulete mabadiliko mapya

    Jibu

    Barcelona wamepata jembe

    Jibu

    Ngoj tuone

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Barca walikuwa wanaenda kumpoteza Griezman thanx kwa Koeman kwa kutaka kumuibua tena tuombeee afanye na kwa dembele na coutinho

    Jibu

    Habar njema

    Jibu

    Na mtabili km star ajaye pale barc endapo mess ataondok

    Jibu

    Hakitaharibika kitu hapo. Akiwepo Griezmann mambo yatakuwaa fresh

    Jibu

    Ni Jambo zuri sana

    Jibu

    Afadhali labda Barcelona italudi kwenye ubora wake!!

    Jibu

    Ni Jambo jema

    Jibu

    Na hii ndio sababu inayomfanya abakie barca licha ya kuhusishwa kurudi altetical.

    Jibu

    Dash back ishapotea tayari kawa wanataka Griezmann awe ngunzo imara itabidi watafutwe wachezaji wazuri wakumpa ushirikiano la sivyo ndiyo basii watabakia jina tu

    Jibu

    Griezman ni mchezaji mzuri Sana pia hataisaidia Barcelona kwa kiwango kikubwa

    Jibu

    Nijambo jema

    Jibu

    Ni kwel

    Jibu

    Griezman amehakikishiwa namba na alikuwa na hatihati ya kuondoka ndio maana amefurahia ujio wa Koeman ambaye gazeti moja liliwahi kumwelezea kama Trump wa Uholanzi#meridianbettz

    Jibu

    Sanaa

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.