Mshambuliaji wa Borrusia Dortmund, Earling Haaland ameendeleza rekodi bora katika ligi ya mabingwa barani ulaya walipo tinga robo fainali baada ya kuwaondoa Sevilla.
Haaland amefikisha magoli 20 katika michezo 14 aliyoicheza katika mashindano ya ulaya, katika mchezo dhidi ya Sevilla ulioisha 2-2.

Erling alifunga magoli mawili na kuisaidia timu yake kufuzu kwa magoli 5-4. Akiwa amefunga jumla ya magoli 10 katika ligi ya mabingwa akiwa na Dortmund.
Haaland amekuwa mchezaji wa kwanza kufikisha magoli 20 kwa haraka zaidi katika ligi ya mabingwa, akifanya hivyo katika mechi 14. Pia akiwa mchezaji mdogo kufunga mechi 6 mfululizo za ligi ya mabingwa.
Pia akichukua nafasi ya Ole Gunnar Solskjaer kuwa mfungaji bora wa muda wote wa Norway katika mashindano hayo. wakati huo akiwa mchezaji wa kwanza kufunga magoli mawili au zaidi katika mechi 4 mfululizo.
Ni Burudani Iliyokithiri na Mkwanja Nje Nje Katika Mchezo Halisi wa Chicago Gold.
Fanikisha malengo yako bila kuumiza kichwa, tengeneza mkwanja bila wasiwasi na kasino ya Meridianbet. Jiunge sasa Ufurahie Chicago Gold kasino.



warda
Haaland Anajua sana namuona kama CR7 Wadae
Venerose
Dortumund wapo vinzur
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri
Hopemwaikuka
Kijana yuko vzur
Sarah
Vizuri
Issa
Yupo vzur