Mshambuliaji wa klabu ya Manchester City Earling Haaland kuwakosa Luton Town leo katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza unaotarajiwa kupigwa katika dimba la Etihad.
Haaland anaripotiwa kupata majeraha ambayo yatamfanya kukosa mchezo wa leo dhidi ya klabu ya Luton Town, Huku ikiwa haijafahamika mshambuliaji huyo kinara atakaa nje ya uwanjwa kwa muda gani.
Klabu ya Manchester City leo watashuka dimbani wakimenyana na Luton Town baada ya kucheza michezo minne bila kupatia matokeo ya ushindi, Huku wakienda kucheza kwenye mchezo huo bila ya mshambuliaji wao namba moja.
Mshambuliaji Haaland amekua mchezaji muhimu sana ndani ya kikosi cha Manchester City, Hivo kukosekana kwake katika mchezo wa leo nmi pengo kubwa kwa klabu hasa ukizingatia kipindi hicho ambacho hawajapata matokeo ya ushindi mfululizo.
Mchezo wa leo unaweza kua mchezo mgumu kwa Manchester City kutokana na muenendo wa matokeo yao kwenye michezo ya hivi karibuni, Lakini pia unaweza kuwapa nguvu ya kupambania kutetea taji lao kama watashinda mchezo huu.

