Kiungo wa Klabu ya Manchester City, Rodri anaendelea kuuguza majeraha aliyoyapata kwenye mchezo wa kombe la Dunia la vilabu huku ikipambana kuhakikisha anakua sawa kuelekea msimu mpya wa ligi kuu Uingereza. Kiungo huyu wa kati alikosa sehemu kubwa ya msimu wa 2024/25 baada ya kupata jeraha kubwa la kuvunjika kwa ligamenti ya mbele ya goti mwezi Septemba mwaka jana.

Majeraha hayo yalikuja wakati ambao Manchester City wanategemea mshindi huyo wa Ballon d’Or 2024 kusaidia kuirejesha timu yao kwenye kiwango cha juu katika ligi ya England baada ya msimu mgumu uliopita.
Hata hivyo, Guardiola amefichua kuwa Rodri alipata jeraha jingine katika mchezo wa mtoano wa robo fainali dhidi ya Al-Hilal, uliofanyika Marekani. “Rodri anaendelea kuimarika, lakini alipata jeraha kubwa katika mchezo wa mwisho dhidi ya Al-Hilal,” alisema Guardiola.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

“Ameonyesha maendeleo mazuri katika mazoezi ya siku za hivi karibuni. Tunategemea baada ya mapumziko ya kimataifa atakuwa katika hali nzuri ya kucheza. Katika mechi hizi, anaweza kupata dakika za kucheza, lakini jambo muhimu ni asije akajitonesha ili tusije tukampoteza tena kwa majeraha. Tutajitahidi sana kuhakikisha anarejea salama. Ameanza kufanya mazoezi pamoja nasi kwa kipindi cha hivi karibuni, na hilo ni jambo la kupongeza.”
Iwapo hali hiyo itaendelea, basi Rodri atakosa mechi tatu za mwanzo za Premier League msimu huu. Manchester City wanatarajia kuanza kampeni zao kwa kucheza dhidi ya Wolves ugenini, kisha kucheza nyumbani dhidi ya Tottenham kabla ya kwenda kucheza na Brighton. Kwa upande wa timu ya taifa ya Hispania, Rodri atakuwa na nafasi ya kucheza katika mechi mbili za kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Bulgaria na Uturuki mwanzoni mwa mwezi Septemba.

Kwa sasa, mshindi huyo wa Ballon d’Or anahitajika kupona kikamilifu ili kuweza kuendelea kutoa mchango wake mkubwa kwa klabu na taifa katika mashindano yanayokuja.

