Beki wa kati ndani ya kikosi cha Yanga kinachofundishwa na Sead Ramovic, Ibra Bacca amewafunika mabeki wote Bongo kwenye rekodi za kuwa na ushkaji na nyavu kwa kufunga mabao mengi ndani ya ligi licha ya kwamba yeye ni mlinzi.

Kutoka Ligi Kuu Bara inayodhaminiwa na NBC ambayo ni namba nne kwa ubora barani Afrika, Ibrahim katupia mabao manne kwenye ligi na kinara wa utupiaji ni Elvis Rupia wa Singida BlacK sTARS huyu ni mshambuliaji kafunga mabao 8.
Anashikilia rekodi ya kufunga bao lililopewa jina la mkono wa ajabu ilikuwa kwenye mchezo dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo huo Bacca alitupia mabao mawili.
Ilikuwa ni Desemba 22 2024 mchezaji huyo alifunga mabao hayo ilikuwa Uwanja wa KMC, Complex bao la kwanza alifunga dakika ya 42 na bao la pili la mkono wa maajabu alifunga dakika ya 83.


