Klabu ya Inter Milan wapo tayari kumuuza mshambuliaji wao, Lautaro Martinez kwa €90m msimu huu wa joto wakati Liverpool, Atletico Madrid na Borussia Dortmund miongoni mwa timu zinazomuwania.

Taarifa zinasema, Lautaro Martinez ndiye mchezaji anayewezekana kuwekwa kwenye soko la uhamisho mwishoni mwa msimu huu ili kusaidia kufadhili usajili wa wapya zaidi.
Martinez alisajiliwa Euro milioni 25 mnamo Julai 2018 kutoka Klabu ya Racing na kuongeza mkataba wake mnamo Oktoba utakaodumu hadi Juni 2026.
‘El Toro’ amefunga mabao 12 katika mechi 33 za kimashindano akiwa na Inter Milan msimu huu, ameshindwa kufunga goli katika mechi saba zilizopita za Serie A.
Kulingana na taarifa mbalimbali bei ya Lautaro Martinez itakuwa takriban €90m, ikiwa imepunguzwa kwa kiasi kikubwa kutoka kwenye kifungu cha mkataba wake cha €110m.
Meridianbettz na Aviator wanakupa mchongo wa kuibuka na iPhone 12 katika kasino ya Aviator itakayodumu kwa siku 7. Kuwa rubani wa Aviator na ujishindie!


