Manchester United inamuwinda Mkurugenzi wa Michezo wa Atletico Madrid

Klabu ya Manchester United baada ya kuachana na mkurugenzi wake wa michezo raia wa kimataifa wa Uingereza Dan Ashowrth inaelezwa kwasasa wanamfukuzia mkurugenzi wa michezo wa Atletico Madrid ya nchini Hispania.

Mkurugenzi wa michezo wa klabu ya Atletico Madrid kwasasa ni raia wa kimataifa wa Italia ambaye anaitwa Andrea Berta ambaye ana zaidi ya miaka 10 ndani ya klabu hiyo nchini Hispania, Kwani alijiunga na klabu hiyo ya nchini Hispania mwaka 2013 mwezi Mei na ameendelea kusalia klabuni hapo mpaka sasa akiwa amefanya kazi kubwa sana akishirikiana na kocha Diego Simeone.

 

Andrea Berta alijiunga na Atletico Madrid kama mkurugenzi wa ufundi ndani ya klabu hiyo mpaka pale alipochukua nafasi ya ukurugenzi wa michezo klabuni hapo mwaka 2017,  Muitaliano huyo mtaalamu wa michezo amesimamia miradi mbalimbali ndanmi ya klau hiyo ya nchini Hispania na ikawa yenye mafanikio makubwa jambo ambalo limefanya Man United kuvutiwa nae.

Manchester United wanamuona Berta kama mtu sahihi ambaye anaweza kuvaa viatu vya Dan Ashworth ambaye amedumu ndani ya klabu hiyo muda wa miezi mitano tu na kuondolewa,Man United wanamuona Berta ni mtu aliyebobea kwenye sekta ya michezo na mwenye uzoefu wa kutosha kutokana na kazi kubwa mabayo ameifanya ndani ya klabu ya Atletico Madrid kwa miaka zaidi ya kumi.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.