Mlinzi wa timu ya Chelsea Marcos Alonso anaacha kupiga goti katika michezo yote inayokuja kwa ajiri ya kupinga ubaguzi wa rangi na badala yake kusimama kuonyesha kidole kweye nembo ya kupinga ubaguzi.
Crystal Palace winga Wilfred Zaha alikuwa mchezaji wa kwanza kuacha kupiga goti katika ligi kuu ya Uingereza na sasa Marcos Alonso anaungana nae.

Marcos Alonso linukuliwa akisema “napinga vikali ubaguzi wa rangi na napinga ubaguzi wa aina yeyote”
“Napendelea kufanya kwa njia hii, na nasema kwa uwazi napinga ubaguzi na namuheshimu kila mtu.” aliongezea
Utaratibu wa kupiga goti kabla ya mpira kuanza ilianza lipindi kile cha kampeni ya ‘black lives matter’ baada ya kusima kwa ligi kuu ya Uingereza kwa siku 100 kutokana na mripuko wa uviko-19 mwaka 2020.
Ni wakati wa ushindi mkubwa ukiwa na kasino bomba ya Lock a Luck, meridianbet wanakupa sababu ya ushindi, funga bahati yako ya ushindi ukiwa na mabingwa.


