Messi Asema Qatar 2022 Itakuwa Kombe Lake la Mwisho la Dunia

Nahodha wa timu ya Taifa ya Argentina Lionel Messi amethibitisha kuwa  Qatar 2022 itakuwa ndilo Kombe lake la mwisho la Dunia, ambapo michuano hiyo inatarajiwa kuanza Novemba mwezi huu.

 

Messi Asema Qatar 2022 Itakuwa Kombe Lake la Mwisho la Dunia

Mshambuliaji huyo wa Paris Saint-Germain atajaribu kunyanyua kombe hilo kwa mara ya kwanza baada ya kuisaidia nchi yake kushinda Copa America mwaka jana. Mchezaji huyo mwenye miaka 35 anasema kuwa hatacheza Kombe lingine la Dunia kufuatia onyesho la Qatar mwaka huu.

Aliiambia Star+: “Hii ni Kombe langu la mwisho la Dunia, hakika, ndio.”

Messi ambaye mpaka sasa ameshinda tuzo ya Ballon d’Or mara saba haamini kwamba Argentina itashiriki michuano hiyo ikiwa kama timu inayopigiwa chapuo kubwa na  watu kubeba kombe hilo.

Messi Asema Qatar 2022 Itakuwa Kombe Lake la Mwisho la Dunia

Aliongeza: “Sijui kama sisi ni wapenzi wakuu, lakini Argentina yenyewe daima ni mgombea kwa sababu ya historia yetu, kwa sababu ya maana yake, na zaidi jinsi tulivyofuzu.

Lionel anaendelea kusema kuwa timu yao sio kipenzi cha watu, kuna timu zingine ambazo ziko juu yao, lakini wapo karibu sana. Wapo kwenye kundi lenye nguvu sana na baada kwenye kombe la dunia hivyo lolote linaweza kutokea.

Messi anaona mambo sawa kutoka kwa kundi na lile la 2014, hawawezi kusubiri kukusanyika pamoja. Kombe la Dunia la 2014 ndilo ambalo alikaribia kulichukua, huku Argentina ikipoteza mbele ya Ujerumani katika fainali. Alisema;

“Ninajisikia vizuri kimwili, niliweza kufanya pre-season nzuri sana mwaka huu ambayo sikuweza kufanya mwaka uliopita, kwa sababu ya jinsi ya kuhamia PSG ilivyotokea. Nilianza kucheza kwa kuchelewa, na msimu tayari ulikuwa umeanza.”

Messi Asema Qatar 2022 Itakuwa Kombe Lake la Mwisho la Dunia

Messi alicheza mechi yake ya kwanza ya Kombe la Dunia nchini Ujerumani mwaka wa 2006 na pia ameshiriki katika matoleo matatu yaliyopita ya michuano hiyo.

Argentina wataanza harakati zao za kutawazwa mabingwa kwa pambano la Kundi C dhidi ya Saudi Arabia kwenye Uwanja wa Lusail mnamo Novemba 22 kabla ya kumenyana na Mexico na Poland.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.