Kiungo wa klabu ya Arsenal raia wa kimataifa wa Ghana Thomas Partey anatarajia kukosa mchezo wa kesho dhidi ya Manchester United baada ya kupata majeraha.
Kiungo Thomas Partey anaukosa mchezo wa kesho kutokana na majeraha ambayo hayajabainishwa mpaka sasamna klabu ya Arsenal, Huku ikielezwa inawezekana akakaa nje ya uwanja kwa muda zaidi.
Klabu ya Arsenal imepata pigo kutokana na kumosa kiungo huyo katika mchezo wa kesho dhidi ya Man United, Kwani mchezo wa kesho utakua mchezo mgumu zaidi na kiungo huyo amekua moja ya wachezaji muhimu ndani ya Arsenal.
Kiungo huyo raia wa kimataifa wa Ghana amekua akiandamwa na majeraha mara kwa mara tangu atue ndani ya klabu ya Arsenal hii imemfanya kukosa michezo mingi na klabu hiyo.
Kukosekana kwa Partey katika mchezo wa kesho dhidi ya Manchester United kesho itakua moja ya changamoto kubwa kwa Arsenal, Lakini kocha Mikel Arteta anahitajika kuja kitofauti na kuhakikisha anatafuta mchezaji mwingine wa kuvaa viatu vya kiungo huyo kesho.

