Kocha mkuu wa Chelsea Graham Potter ameongea kuhusu mkataba wa kiungo wa timu hiyo N’Golo Kanté ambapo mkataba wake unamalizika mwezi Juni huku bado kukiwa hakuna mwafaka wa mchezaji huyo na timu yake.

Potter amesema kuwa jambo zuri kwasasa ni kumsaidia kuwa fiti na bado kiungo huyo ana safari ndefu ya kwenda mbeleni .
Kocha huyo ambaye mpaka sasa hajapoteza mchezo wa aina yoyote amesema kuwa lazima wahakikishe mchezaji huyo anapata matibabu sahihi wakati anafurahia soka lake na pia wanaweza kufikiria kuhusu mkataba wake.

Kante ambae ni mshindi wa Kombe la Dunia mwaka 2018 na timu yake ya Ufaransa, taarifa za mwanzo zilisema kuwa anahitaji mkataba mrefu kwani Koulibaly ana mkataba mrefu kwanini yeye asipewe mkataba huo.
The Blues wanasita kutoa mkataba mrefu kwa kiungo huyo kutokana na umri wake kuwa mkubwa miaka 30 si haba lakini pia kupata majeraha ya hapa na pale yanachangia pia timu hiyo kuhofia kumpa mkataba mrefu halafu aumie.

The Blues leo, watakuwa nyumbani Stamford Bridge kuwaalika Manchester United ya Erik Ten Hag huku msimu uliopita kwenye ligi waligawana pointi moja moja mechi zote mbili.

