Imedaiwa kuwa klabu ya soka ya Arsenal imeapa kumpa adhabu kali mchezaji mshambuliaji wao matata, Alexandre Lacazette! Hii ni mara baada ya kuvuja kwa taarifa kuwa staa huyo ambaye ni mzaliwa wa nchini Ufaransa alionekana akivuta gesi ya Nitrous Oxide ambayo ni maarufu kama ‘Laughing Gas’ iliyokuwa imejazwa ndani ya puto alilokuwa nalo.
kwa mujibu wa gG=azeti la Daily Star la nchini Uingereza lililochapisha makala zenye picha zilizoonesha Lacazette akiwa na puto lenye gesi hiyo mdomoni mwake. Baadaye, mchezaji huyo wa zamani wa Olympique Lyon, Ufaransa aliwatumia wanasoka wenzake wa Arsenal video iliyochukuliwa akivuta gesi hiyo kupitia mitandao yao ya kijamii.
Ingawa msemaji wa Arsenal ameshikilia kwamba tukio hilo ni suala kibinafsi litakaloshughulikiwa na klabu katika kiwango cha ndani kwa ndani, huenda Lacazette akapata adhabu kali.
Kwa sasa ni juma moja pekee limepita tangu Lacazette awe mmoja kati ya wachezaji wengine wa Arsenal waliovunja kanuni mpya za afya zinazodhibiti maambukizi zaidi ya virusi vya Corona. Lacazette ambaye ana umri wa miaka 28 kwa sasa alionekana akiwa karibu sana na mwanamume mmoja aliyekuwa akimuoshea gari lake jijini London!
Kwa kufanya jambo hilo akawa amevunja kanuni inayotaka mtu kusimama ama kukaa umbali wa hadi mita mbili kati yake na mwingine wa jirani yake. Tusubiri kuona itakavyokuwa.
Ernest
Vituko hivi vya wachezaji ambao sisi tunawaita professional players.
Mwanaidi
Ni lazima awajibikie adhabu yake so akae asubirie itakavyoamuliwa
Salma
Sheria ifatwe
mathayo sonje
Haya marungu msimu huu yamekua kama fasheni sasa maana kila kukicha tunapata habari tofauti au wanatafuta kiki??, sema nao arsenali washamchoka lakazet maana kuna tetesi toka mwanzo za kuuzwa kwke
Tahiya
Anastahili adhabu
Asha
Sheria na haki itendekeh Asante meridian kwa update
Povel
Sheria ifuate mkondo wake thanks meridian kwa update
Lombo
gud newz
mwakalosi
Ulaya wana sheria nyingi na kali huku kwetu wachezaji unapishana nae bar au kwenye ndondo akivuta bangi
winfrida
acha apate adhabu ukijifanya mjuaji faida yake ndo iyo
Mwajuma
Anastahili adhabu ili iwefundisho kwa wengine
Neema hassan
Adhabu kali ichukuliwe dhidi yake
Frank Patrick
Wenzetu wanafuatilia sana aisee
Gabriel
Atakuwa ameonewa
SADICK
Ni lazima mchezaji wa kulipwa kuheshimu taratibu zilizowekwa na Club kulinda hadhi yako na Club unayotumikia. Wacha akutane na rungu la Club.
Adelta
Ni kweli ukikosea lazima upewe adhabu
Warda
Jamaa huwa anabahati mbaya sana#Meridianbettz
Emmy cleopa
Sheria ifatwe hanastaili adhabu
#meridianbettz
Asia Abdy
Duuh pole yake
felister
adhabu lazima ili iwe funzo kwa wengine
Tatu
Kweli anastahili adhabu
Kenani
Ninlazma afate Sheria na misingi ya club inasemaje la sivyo anastahili adhabu
Furahav
Mmh majanga.
Ester mmakasa
Duuh!ana shutuma nzinto sana inabidi sheria ifwate mkondo wake kama kavunja kanuni.
Shafii
Asanteni meridianbet habari za mchezo hapahapa
aisha
Adhabu inamuhusu
Mariam mtandama
Habari mjema
Issa
Apate onyo ili iwe fundisho kwa wachezaji wengine pia