Mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah amerejea mazoezini kwaajili ya mchezo wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) utakaowakutanisha na Atalanta ya Italia uwanjani Anfield leo.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 alikosa mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) iliyoshuhudia Liverpool wakiibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Leicester City uwanjani Anfield Jumapili iliyopita.

Salah alikosekana katika mchezo huo kutokana na ugonjwa wa Covid-19 alioupata wakati akiwa katika kambi ya timu ya taifa ya Misri iliyokuwa ikicheza na Togo kwenye mechi mbili za kufuzu kwa fainali za Kombe la Afrika (AFCON) mnamo 2022.
Katika mechi iliyopita ya UEFA, Liverpool waliwafunga Atalanta kwa magoli 5-0 jijini Bergamo, Italia na mechi ya leo itakuwa marudiano katika uwanja wao wa nyumbani Anfield, Uingereza.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.



magdalena
safi salaah kurudi uwanjani
Ester jackson
Hii mechi itakuwa good sana mana nataka kuona makali ya salah ya koje alipotoka karantini
Fatina mfingi
Itakuwa bonge la mechi kam salah hatakuwep
Khadija
Amefanya jambo zuri sana kurudi uwanjani
Rahma
Safi analudi tena uwanja
Dorophina
Habari njema hizi kwa mashabiki wa liverpool
Sauda
Karibu sana Liverpool
Shakila mrope
Good new
Mwajumah
Itakua si ya kukosa hii kama Sarah ndan ya dimba
Caroline
Mo Salah tunakuaminia
Sania
Karibu tena Mo Salah
Nasra
Tunakupokea kwa mara nyingine tena
Povel
Habar njema kwa mashabik wa liverpool kwa uwepo wa mo salah katika mchezo wa leo
Saupha mohamed
No salah mtu makini
Issa
Salah amekua mchezaji ambae ni muhim kwa liverpool kwa muda mrefu
aisha
Bora salah yuko fiti maana tulimmic sana
Sadick
Jambo la kuvutia ni kwamba tunaanza kuishi na corona kama kawaida tofauti na awali tulivyokuwa tunaogopa mno. Karibu Dimbani Mo Salah
Hopemwaikuka
Jambo jema
Tatu
Habari nzuri kwa mashabiki wa salaa
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri Sana mapambano yataenderea kwa salaa
Sarah
Karibu Tena salaa
warda
Salah mnyama mkali