Ripoti zisizo rasmi zinasema klabu za Simba SC na Azam FC zipo katika kinyang’anyiro cha kuwania saini ya kiungo mkabaji, Khalidi Aucho aliyemaliza mkataba na timu yake.

Kiungo wa Kimataifa wa Uganda, 🇺🇬 Khalid Aucho (27) juzi Ijumaa amethibitisha kuondoka katika klabu ya Misr El Makkasa ya Ligi Kuu ya Misri baada ya kuitumikia kwa miaka miwili.
Kiungo huyo wa zamani wa Baroka FC na Gor Mahia amesema katika siku chache zijazo ataeleza ni wapi anatarajia kucheza msimu huu.
Inaelezwa kuwa klabu ya Simba SC iliishaingia makubaliano ya awali na nyota huyo lakini kwasasa matajiri wa Chamazi wameonyesha nia ya kumuhitaji hili kwenda kuziba nafasi ya Ally Niyonzima.
SHOOT! mchezo unaokupa nafasi ya kupambania ushindi wako mkubwa kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet! Usisubiri hii, jiunge sasa kufurahia ushindi!



Sarah
Simba wako vizuri
Sania+mapua
Mwenye kisu kikali ndiye atayekula nyama