Tetesi za Soka Barani Ulaya.


 

Tetesi za zinasema Manchester United huenda wakawasilisha dau la kumnunua kiungo wa kati wa West Ham Declan Rice, 21, japo mchezaji huyo anadhaniwa kutaka kujiunga na Chelsea endapo ataamua kuondoka Hammers.

Tetesi zinasema Wolves inamfuatilia mshambuliaji wa Liverpool na Ubelgiji Divock Origi, 25, ambaye huenda akaruhusiwa kuondoka mwezi Januari.

Manchester United wanashughulikia mchakato wa Marcos Rojo kuondoka klabu hiyo mwezi Januari, huku Newcastle wakipania kumsajili kwa mkopo mlinzi huyo wa Argentina aliye na umri wa miaka 30.

 

Liverpool wamemuongeza mchezaji Roma wa safu ya kati na nyuma Roger Ibanez katika orodha ya walinzi wanaosakwa kujaza pengo lililoachwa na mchezaji wa kimataifa wa Uholanzi Virgil van Dijk, 29, aliyejeruhiwa na huenda wakawasilisha dau la £30m kumnunua.

Mgombea wa Rais wa Barcelona Victor Font amesema hatarudia makosa yaliyofanywa na watangulizi wake kutangaza nia ya kuwanunua wachezaji nyota licha ya kuhusishwa na tetesi za kumnyatia mshambuliaji wa Borussia Dortmund na Norway Erling Haaland, 20. Lakini anapanga kumshawishi Lionel Messi, 33, kusaini mkataba mpya.

Kiungo wakati wa Hungary Dominik Szoboszlai, 20, anayenyatiwa na Arsenal, amekamilisha uhamisho wa RB Leipzig kutoka klabu dada ya Red Bull Salzburg, na anatarajiwa kujiunga nayo mwezi Januari baada ya kusaini mkataba wa miaka minne na nusu.

 

Szoboszlai baada ya kukamilisha usajili wa RB Leipzig

Tetesi zinasema Arsenal inakaribia kukamilisha usajili wa mchezaji wa safu ya kati na nyuma ya Hertha Berlin Omar Rekik baada ya mlinzi huyo aliye na umri wa miaka 18-year-kuwasili mjini London siku ya Alhamisi.

Napoli inataka angalau £14m kumuuza mshambuliaji wa Poland Arkadiusz Milik mwezi Januari Januari licha ya mchezaji huyo kunyatiwa na Juventus na Atletico Madrid.

Mkufunzi wa Everton Carlo Ancelotti ana matumaini ya kukamilisha mkataba wake katika klabu hiyo kwa ushindi wa mataji katika kipindi cha muda atakaokuwa hapo hadi mwisho wa msimu wa 2023-24.


BURUDIKA NA WANYAMAPORI WAKIIMBA NA KUPIGA VYOMBO VYA MUZIKI!

Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, furahia mchezo wa Forest Rock. Hapa utaburudika na umahiri wa wanyapori wanaoimba na kutumia vifaa vya muziki wa rock. Burudika huku ukijiwekea nafasi ya kutengeneza pesa ndefu kupitia Meridianbet!!

INGIA MCHEZONI!

15 Komentara

    Man u wakimpata huyo jamaa itakua poa

    Jibu

    Hii ni makala nzuri yenye maelezo mazuri kwa kutuelimisha

    Jibu

    Asant kwa makala meridian bett pesa njenje

    Jibu

    Asante kwa makala meridian bet

    Jibu

    Man u wajitahidi wampate tu

    Jibu

    Man u wakimpata rice itakuwa poa sana dogo yupo vizuri

    Jibu

    man wajitahidi

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Vzr

    Jibu

    Man U wajitaidi wakimpata itakuwa poa

    Jibu

    Good

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Mpo vizur meridian bet

    Jibu

    Man Utd wajitahidi

    Jibu

    Safi

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.