Pengine wengi hawakutegemea hili lakini ni Jurgen Klopp aliyebeba tuzo ya kocha bora wa mwaka kutoka FIFA.
Jurgen Klopp alikuwa akipambania tuzo hiyo na Hans Flick (Bayern Munich) pamoja na Marcelo Bielsa (Leeds United).
Baada ya kuiongoza Liverpool kutwaa taji la EPL msimu uliopita na kuondoa ukame wa kubeba kombe hilo kwa miaka 30, Klopp amebeba tuzo ya kocha bora wa FIFA kwa mara ya pili mfululizo.
Mwaka jana Klopp alibeba tuzo hiyo baada ya kuiongoza Liverpool kutwaa kombe la Ligi ya Mabingwa – UEFA.
Ukilinganisha mafanikio ya Klopp na wapinzani wake katika kipengele hicho, huwezi kumdhania Mjerumani huyu kama angebeba tuzo hiyo.
Hans Flick alitwaa mataji yote ya Ligi ya soka Ujerumani pamoja na UEFA alipoiongoza Bayern Munich na kumaliza msimu uliopita kwa kubeba makombe matano.
Marcelo Bielsa alifanyakazi kubwa kunako mashindano ya Championship nchini Uingereza na kuifaipandisha Leeds United kwenye ligi kuu – EPL baada ya kuibuka vinara wa Championship.

Usilolijua ni kwamba, wakati mchakato wa kutafuta wagombea wa tuzo hizi unaanza (Julai 20,2019) , Hans Flick hakuwa kocha mkuu wa Bayern Munich bali alikuwa ni msaidizi wa Niko Kovac na hivyo hakuwa ametimiza muda unaotakiwa kuzingatiwa ili kupata tuzo ya kocha bora.
Hata Jurgen Klopp mwenyewe alitegemea Flick angepatiwa heshima hiyo lakini haikuwa hivyo.
Akizungumza wakati wa utoaji wa tuzo hizo, Klopp alisema ” Nimeshtuka. Nilikuwa nimekaa hapa kwa sababu mwaka jana nilishinda kwa hiyo ninawapa heshima watu wote kwa kuwa nilichaguliwa kuwania (tuzo) na nimejitokeza kwa lolote.”
Baada ya kuambiwa kuwa yeye ndiye Kocha Bora wa FIFA wa Wanaume, Klopp alisema “Hapana, lakini nimeshinda tuzo, hiyo inatosha.”
Klopp anashikilia usukani wa msimamo wa EPL kwa alama 3 zaidi ya Tottenham ya Jose Mourinho.
BURUDIKA NA WANYAMAPORI WAKIIMBA NA KUPIGA VYOMBO VYA MUZIKI!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, furahia mchezo wa Forest Rock. Hapa utaburudika na umahiri wa wanyapori wanaoimba na kutumia vifaa vya muziki wa rock. Burudika huku ukijiwekea nafasi ya kutengeneza pesa ndefu kupitia Meridianbet!!



Hopemwaikuka
Congrats to u Jurgen klopp
Adelta
Jurgen klopp ni kocha mwenye mfano mzuri wa kuigwa
Shakila mrope
🔥🔥🔥
Rahma
Nic
Sarah
Ongera yake jurgen
Dorophina
Hongera mwamba klopp
Issa
Klop kocha
felister
klopp 👏
Janeflora malisa
Safi
Lydia Emmanuel Magoti
Safiii sana
lombo
vzr
Saupha mohamed
Hongera
Caroline
Hongera sana klopp
warda
klopp sasa hivi anajisikia sana
Tatu
Hongera yake
samiah
Pongezi kwake