Tetesi zinasema José Mourinho anataka kumrejesha Tottenham mshambuliaji wa Real Madrid na Wales Gareth Bale, 31.
Tetesi zinasema Beki wa kati wa Paris St -Germain Thiago Silva, 35, ambaye anaondoka kwenye klabu hiyo ya Ufaransa baada ya fainali za michuano ya klabu bingwa Ulaya amepewa ofa na Chelsea.
Kushindwa kufikiwa kwa maelewano binafsi ya mkataba wa Muingereza Jadon Sancho, 20 kumeongeza ugumu wa uhamisho wake kutoka Borussia Dortmund kwenda Manchester United.

Manchester United wanaweza kuipatia Aston Villa mlinda mlango Sergio Romero,33, kama sehemu ya makubaliano ili kumpata kiungo wa kati Jack Grealish, 24.
Tetesi zinasema Chelsea na Atletico Madrid wana mpango wa kumpata winga Federico Bernardeschi, 26, anayekipiga Juventus.
Tetesi zinasema Liverpool inajiandaa kumuuza kiungo Marko Grujic, 24, na winga Harry Wilson, 23, msimu huu.
Chelsea watakamilisha kumsajili kiungo wa kati wa Kijerumani Kai Havertz, 21, wiki hii kwa mkataba wa miaka mitano iwapo wao na Bayer Leverkusen wanaweza kupunguza tofauti ya pauni milioni 18 ya thamani ya mchezaji huyo.

Kiungo wa kati wa Manchester United Mbrazili Andreas Pereira, 24, analengwa na Benfica na Valencia. Pia United imerejesha shauku yao kwa beki wa kushoto Alex Sandro, 29, anayeichezea Juventus
Tetesi zinasema Leeds imekataa ofa ya tatu inayoaminika kuwa takribani pauni milioni 25 kwa ajili ya mchezaji wa nafasi ya ulinzi Ben White, 22.
Tetesi zinasema Tottenham inataka kumchukua mshambuliaji wa Liverpool Rhian Brewster, 21 kwa mkopo.
Wolves wako tayari kusikiliza ofa kubwa kwa ajili ya winga Adama Traore ingawa mchezaji huyo, 24, bado amesalia na miaka mitatu ya kuutumikia mkataba wake.
West Ham inataka kumuuza mshambuliaji Jordan Hugill, 28, msimu huu. Hugill aliutumia msimu uliopita akichezea QPR kwa mkopo.
Fulham imeuliza mustakabali wa mlinzi wa kati wa Barcelona Gerard Pique, 33.

Fulham na Wolves huenda wakachuana na Everton kupata saini ya Kiungo wa kati wa Watford Abdoulaye Doucoure, 27.
Bournemouth wanajiandaa kutoa ofa kwa ajili ya mlinda mlango wa Wigan David Marshall, 35.
Cottagers wameingia pia katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa Bournemouth Muigereza Callum Wilson, 28.
Leeds inatayarisha kitita cha pauni milioni 10 kwa ajili ya winga wa Rangers, Ryan Kent, 23.
Kocha wa zamani wa England Sven Goran Eriksson anajiandaa kuwa kocha mpya wa Jamaica.
Chelsea itafanya mazungumzo na kiungo wa kati Conor Gallagher huku Newcastle na Crystal Palace zote zikionesha nia ya kumsajili msimu uliopita .
Burnley inafanya mazungumzo ya kumsajili kiungo wa Angers, Baptiste Santamaria. Raia huyo wa Ufaransa, 25, alikuwa gumzo kwasababu ya kitita cha pauni milioni 12 na Aston Villa mwaka jana.

Brighton inasema nahodha Lewis Dunk, 28, na mlinzi Ben White, 22, watasalia katika klabu hiyo. Dunk amehusishwa na Chelsea huku Leeds ikiwa inataka kufanya mazungumzo na White.
Arsenal ina matumaini ya kukamilisha makubaliano ya pauni milioni 22 kwa mlinzi wa Lille Gabriel Magalhaes. Everton na Napoli pia nazo zinamnyatia mchezaji huyo wa Brazil, 22.
Drops and Wins!
Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.


Zeiyana
Kwa uwezo alikua nao bale kila clabu inamtamani itakua vizuri akienda Tottenham naona pale Real Madrid hakuna inshu tena
Dorophina
Thiago Ni bora akakubali ofa ya Chelsea
Mwajumah
Bale kwa uwezo aliokua nao Kila clabu inamtamani Bora aende Tottenham tu#Meridianbettz
rama
Maoni:mhh bale umri ushaenda tayari atafute vijana tu
Ernest
Bale kurudi Spurs ni bonge na deal sema Spurs watakuwa na hela?
Fatina mfingi
Asanteh kwa taarifa meridianbet!!
Venerose
Asante kwa taarifa
Nasra
Gud news
Ester jackson
Kwa ofa ambayo bale anatakiwa kwenda Tottenham bora aende mana hapo hapamfaii kabisa real Madrid
Khadija
Asante kwa taarifa
aisha
Real madrid hakuna maajabu ni bora aondoke maana uwezo wake ni mkubwa sana na pia anakipaji cha kufanya mambo mengi ila sio hapo alipo naona kama kipaji chake kinafifia
Mwanahamisi
Gud news
Adelta
Bale kurudi spurs Ni bonge la siku
@meridianbettz
Magdalena
arsenal wekeni dau mmchukue gabriel yupo vizuri sana
Lydia Emmanuel Magoti
Arsenal waweke dau wamchukue jembe Hilo Gabriel yupo vizuri sana
Shan
Habar njema Thiago ni kijana mahiri uwanjan!!
Furahav
Gud news.
Samiah
Gud
Saupha mohamed
Good news
Salma ngende
Habari nzuri
Povel
Habar njema
Amiri Kayera
Safii
Sabrina
Bora Bale aende Spurs Maana madrid washamchoka
Devotha
Habari njema
Janeflora malisa
Good
Theonestina
Habari njema
Latifa juma mohamed
Taarifa njema.
David Pere
Kushindwa kufikiwa kwa maelewano binafsi ya mkataba wa Muingereza Jadon Sancho, 20 kumeongeza ugumu wa uhamisho wake kutoka Borussia Dortmund kwenda Manchester United.
warda
Jose hashidwi na kitu
felister
Bale bora aende zake spurs tu
Tatu
Chelsea kufanya mazungumzo na conor Gallagher
Hope mwaikuka
Zmeeleweka sana
Shafii
Zipo kamili gado Sana.