Tetesi za Soka Barani Ulaya.


Tetesi zinasema José Mourinho anataka kumrejesha Tottenham mshambuliaji wa Real Madrid na Wales Gareth Bale, 31.

Tetesi zinasema Beki wa kati wa Paris St -Germain Thiago Silva, 35, ambaye anaondoka kwenye klabu hiyo ya Ufaransa baada ya fainali za michuano ya klabu bingwa Ulaya amepewa ofa na Chelsea.

Kushindwa kufikiwa kwa maelewano binafsi ya mkataba wa Muingereza Jadon Sancho, 20 kumeongeza ugumu wa uhamisho wake kutoka Borussia Dortmund kwenda Manchester United.

 

Tetesi za Soka Barani Ulaya.

Manchester United wanaweza kuipatia Aston Villa mlinda mlango Sergio Romero,33, kama sehemu ya makubaliano ili kumpata kiungo wa kati Jack Grealish, 24.

Tetesi zinasema Chelsea na Atletico Madrid wana mpango wa kumpata winga Federico Bernardeschi, 26, anayekipiga Juventus.

Tetesi zinasema Liverpool inajiandaa kumuuza kiungo Marko Grujic, 24, na winga Harry Wilson, 23, msimu huu.

Chelsea watakamilisha kumsajili kiungo wa kati wa Kijerumani Kai Havertz, 21, wiki hii kwa mkataba wa miaka mitano iwapo wao na Bayer Leverkusen wanaweza kupunguza tofauti ya pauni milioni 18 ya thamani ya mchezaji huyo.

 

Tetesi za Soka Barani Ulaya.

Kiungo wa kati wa Manchester United Mbrazili Andreas Pereira, 24, analengwa na Benfica na Valencia. Pia United imerejesha shauku yao kwa beki wa kushoto Alex Sandro, 29, anayeichezea Juventus

Tetesi zinasema Leeds imekataa ofa ya tatu inayoaminika kuwa takribani pauni milioni 25 kwa ajili ya mchezaji wa nafasi ya ulinzi Ben White, 22.

Tetesi zinasema Tottenham inataka kumchukua mshambuliaji wa Liverpool Rhian Brewster, 21 kwa mkopo.

Wolves wako tayari kusikiliza ofa kubwa kwa ajili ya winga Adama Traore ingawa mchezaji huyo, 24, bado amesalia na miaka mitatu ya kuutumikia mkataba wake.

West Ham inataka kumuuza mshambuliaji Jordan Hugill, 28, msimu huu. Hugill aliutumia msimu uliopita akichezea QPR kwa mkopo.

Fulham imeuliza mustakabali wa mlinzi wa kati wa Barcelona Gerard Pique, 33.

 

Tetesi za Soka Barani Ulaya.
Gerard Pique

Fulham na Wolves huenda wakachuana na Everton kupata saini ya Kiungo wa kati wa Watford Abdoulaye Doucoure, 27.

Bournemouth wanajiandaa kutoa ofa kwa ajili ya mlinda mlango wa Wigan David Marshall, 35.

Cottagers wameingia pia katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa Bournemouth Muigereza Callum Wilson, 28.

Leeds inatayarisha kitita cha pauni milioni 10 kwa ajili ya winga wa Rangers, Ryan Kent, 23.

Kocha wa zamani wa England Sven Goran Eriksson anajiandaa kuwa kocha mpya wa Jamaica.

Chelsea itafanya mazungumzo na kiungo wa kati Conor Gallagher huku Newcastle na Crystal Palace zote zikionesha nia ya kumsajili msimu uliopita .

Burnley inafanya mazungumzo ya kumsajili kiungo wa Angers, Baptiste Santamaria. Raia huyo wa Ufaransa, 25, alikuwa gumzo kwasababu ya kitita cha pauni milioni 12 na Aston Villa mwaka jana.

 

Tetesi za Soka Barani Ulaya.

Brighton inasema nahodha Lewis Dunk, 28, na mlinzi Ben White, 22, watasalia katika klabu hiyo. Dunk amehusishwa na Chelsea huku Leeds ikiwa inataka kufanya mazungumzo na White.

Arsenal ina matumaini ya kukamilisha makubaliano ya pauni milioni 22 kwa mlinzi wa Lille Gabriel Magalhaes. Everton na Napoli pia nazo zinamnyatia mchezaji huyo wa Brazil, 22.


Drops and Wins!

Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.

Soma Zaidi

33 Komentara

    Kwa uwezo alikua nao bale kila clabu inamtamani itakua vizuri akienda Tottenham naona pale Real Madrid hakuna inshu tena

    Jibu

    Thiago Ni bora akakubali ofa ya Chelsea

    Jibu

    Bale kwa uwezo aliokua nao Kila clabu inamtamani Bora aende Tottenham tu#Meridianbettz

    Jibu

    Maoni:mhh bale umri ushaenda tayari atafute vijana tu

    Jibu

    Bale kurudi Spurs ni bonge na deal sema Spurs watakuwa na hela?

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Kwa ofa ambayo bale anatakiwa kwenda Tottenham bora aende mana hapo hapamfaii kabisa real Madrid

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Real madrid hakuna maajabu ni bora aondoke maana uwezo wake ni mkubwa sana na pia anakipaji cha kufanya mambo mengi ila sio hapo alipo naona kama kipaji chake kinafifia

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Bale kurudi spurs Ni bonge la siku
    @meridianbettz

    Jibu

    arsenal wekeni dau mmchukue gabriel yupo vizuri sana

    Jibu

    Arsenal waweke dau wamchukue jembe Hilo Gabriel yupo vizuri sana

    Jibu

    Habar njema Thiago ni kijana mahiri uwanjan!!

    Jibu

    Gud news.

    Jibu

    Gud

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Habari nzuri

    Jibu

    Habar njema

    Jibu

    Safii

    Jibu

    Bora Bale aende Spurs Maana madrid washamchoka

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Good

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Taarifa njema.

    Jibu

    Kushindwa kufikiwa kwa maelewano binafsi ya mkataba wa Muingereza Jadon Sancho, 20 kumeongeza ugumu wa uhamisho wake kutoka Borussia Dortmund kwenda Manchester United.

    Jibu

    Jose hashidwi na kitu

    Jibu

    Bale bora aende zake spurs tu

    Jibu

    Chelsea kufanya mazungumzo na conor Gallagher

    Jibu

    Zmeeleweka sana

    Jibu

    Zipo kamili gado Sana.

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.