Tetesi zinasema, Manchester United wako mbioni kufanya harakati za mwisho kumsajili mshambuliaji wa Wolves Mreno Ruben Neves, 25, ingawa wanakabiliwa na ushindani kutoka Barcelona.
Manchester United wanahofia gharama uhamisho wa Darwin Nunez huku Benfica wakiwa wameiambia United itawagharimu takriban pauni milioni 100 kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay, 22.
Tetesi zinasema, United imewasiliana na Erik ten Hag kuhusu uwezekano wa kumsajili mlinzi wa Villarreal Mhispania Pau Torres, 25, katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi.
Tetesi zinasema, Liverpool itapokea takriban £25m kwa uhamisho wa Sadio Mane kwenda Bayern Munich, huku mshambuliaji huyo wa Senegal, 30, akipangwa kuchukua nafasi ya Robert Lewandowski.
Aston Villa inaangalia uwezekano wa kumsajili Luis Suarez, 35, ambaye ni mchezaji huru baada ya kuachiliwa na Atletico Madrid. Mshambuliaji huyo wa Uruguay ni mchezaji mwenzake wa zamani wa Villa Steven Gerrard.
Paris St-Germain imemuweka sokoni Neymar, 30, msimu huu wa joto. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil alijiunga na klabu hiyo ya Ufaransa kwa rekodi ya dunia ya euro 222m (£200m) mwaka wa 2017 lakini ameonekana mara chache kutokana na majeraha ya mara kwa mara.
Tetesi zinasema, Mabingwa wa Ligue 1 wamepewa ofa ya winga wa Arsenal na Ivory Coast Nicolas Pepe, 26, na klabu hiyo ya kaskazini mwa London.
Sevilla hawana nia ya kupokea chini ya euro 65m (£55m) kwa mlinzi wa Ufaransa Jules Kounde, 23, huku Chelsea wakitarajiwa kuwasilisha ombi lao hivi karibuni.
Kiungo wa kati wa Croatia Ivan Perisic, 33, amekubali masharti ya mkataba wa miaka miwili na Tottenham, waliokuwa wanachuana na Chelsea na Juventus kupata saini yake.
Roma wako tayari kumpa kandarasi mpya mshambuliaji wa Uingereza Tammy Abraham, 24, huku Arsenal, Newcastle na Aston Villa zikiuliza kuhusu upatikanaji wake.
SHINDA Samsung A32 ukiwa na mchezo wa Aviator kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet! Kwea pipa ukusanye zawadi zako pamoja na ushindi mnono wa mkwanja!