Uongozi wa timu ya Malindi na Kipanga zimekiri kupokea Shilingi 3,000 (elfu tatu) kila mmoja ikiwa ni sehemu ya Mapato baada ya makato (gharama nyingine za Uwanja) kwenye mchezo wao nambari 114 wa Ligi Kuu Soka ya Zanzibar uliochezwa Mei 24, 2021 saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Mao Ze Dong.
Katibu wa timu ya Malindi Mohammed Masoud amesema baada ya kulipwa gharama zote za Uwanja zikabakia shilingi 6,000 ambazo kila timu ikapata shilingi elfu tatu (3,000).
“Mbona hii kawaida kwetu [Ligi Kuu ya Zanzibar] hasa mechi tunazocheza uwanja wa Mao, siku nyingine tunapata 1,000, 500 au hatupati kabisa, kwahiyo hii elfu 3 kwetu wala hatujashangaa”- alisema Masoud.
“Ni kweli na sisi Kipanga tumepata elfu tatu tu, lakini mbona hii kawaida tumeshazoea”-alisema Kiongozi mmoja wa Kipanga ambaye hakutaka jjna kake litajwe.
BONASI YA 50% KILA SIKU KATIKA KASINO ZA EVOPLAY HAPA MERIDIANBET.
Meridianbet na Evoplay Kasino wanakupa bonasi ya 50% ya kiasi utakachoweka katika akaunti yako leo. Unasubiri nini ni wakati wa kupiga pesa sasa na Mabingwa.
Duh!!!
Mhhh