Arteta Ailaumu Arsenal Kwa Kupata Ushindi Mdogo

Kocha mkuu wa Arsenal Mikel Arteta ameilaumu Arsenal kwa kupata ushindi mdogo kwenye mchezo wao wa mwisho kwenye michuano ya Europa ambapo walikuwa wakikipiga dhidi ya Zurich.

 

Arteta Ailaumu Arsenal Kwa Kupata Ushindi Mdogo

Arsenal ndio vinara wa kundi hilo wakiwa na pointi 15 baada ya kushinda mechi zao 5 na kupoteza mchezo mmoja huku wakifuatiwa na PSV mwenye pointi 13. Vijana wa Arteta wameshinda mechi 9 za nyumbani katika mashindano yote msimu huu, ukiwa ni muda mrefu zaidi kushinda mwanzoni mwa kampeni tangu 2009-10.

Bao hilo lilifungwa na Kieran Tierney katika kipindi cha kwanza cha mchezo, na mpaka kukamilika kwa dakika hizo 90 ndio bao liliipatia alama 3, huku Arteta akisema kuwa timu yake ilikuwa na makosa katika sehemu za mwisho za mchezo licha ya matokeo hayo.

Arteta Ailaumu Arsenal Kwa Kupata Ushindi Mdogo

Bao hilo linakuwa ni la tatu kwa mchezaji huyo kwenye Ligi ya Europa moja ambapo ni dhidi ya Celtic na kwenye ligi mabao mawili.

Beki huyo wa kushoto amelazimika kucheza nafasi ya chini kwa Tomiyasu kwa sehemu kubwa za msimu lakini alisisitiza kuwa kiwango chake cha uchezaji hakitashuka, iwe kwenye kikosi cha kwanza au la.

Kocha huyo alisema kuwa; “Siku zote tunajaribu kuanza kwa kasi zaidi. Tuna mpinzani ambaye ana jambo la kusema kwenye mchezo, tulifanya mchezo kuwa mgumu katika dakika 15, 20 zilizopita.”

Arteta Ailaumu Arsenal Kwa Kupata Ushindi Mdogo

Hakuishia hapo tu, alisema kuwa kuhusu kuumia kwa Tomiyasu ambaye ni mchezaji wa Kimataifa wa Japan kunawapa wasiwasi na pia hakusema kuwa atarejea muda gani, pia wikendi hii watacheza Dabi ya London dhidi ya Chelsea.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.