Mikel Arteta Kurudi Sokoni Tena

Kocha wa klabu ya Arsenal Mikel Arteta baada ya kukamilisha sajiri tano mpaka sasa bado ameweka wazi kuwa anatarajia kurudi tena sokoni ili kufanya maboresho ya kikosi chake.

Mpaka sasa Mikel Arteta ndie kocha aliyetumia kiasi kikubwa kwenye soko la usajiri ambapo ametumia takribani  £120million, japo kiwango hicho kinaweza kuzidi.

Akizungumza kwenye ushindi wa 4-0 dhidi ya Chelsea, alinukuliwa akisema, ” unaweza kuona kwamba bado tuna upungufu wa baadhi ya nafasi kwa jinsi tunavyohitaji kucheza, tunajaribu kulielezea hili.” Alisema Mikael Arteta

Pia kuna tetesi kuwa kuna wachezaji kadhaa wa klabu ya Arsenal wanaweza kuoneshewa mrango wa kutokea kwenye msimu huu waliwemo Bernd Leno, Hector Bellerin, Pablo Mari, Lucas Torreira na Nicolas Pepe.

 

Acha ujumbe