Jangwani: Katika kujiweka sawa kuelekea Ligi kuu ya wanawake Tanzania Bara, Timu ya wanawake ya Yanga ‘Yanga Princess‘ leo imecheza mchezo wa kirafiki dhidi ya JKT Queens na kuibuka na ushindi wa mabao 3-1.

Mchezo huo ulipigwa kwenye dimba la Chuo cha Sheria jijini Dar Es Salaam ambapo mchezo huo wa leo unakuwa ni wa pili kucheza, baada ya ule uliochezwa wiki iliyopita kwenye dimba la Uhuru na wakali wa Jangwani Yanga Princess waliibuka na Ushindi wa wa bao 1-0
Kwa ushindi huu wa leo unaifanya timu hiyo ya wanawake ya Yangawenye makao makuu yao Jangwani kuwa na rekodi nzuri za ushindi, kwani wanakuwa wameshinda mechi 4 na kupoteza 1, kati ya tano walizocheza.
Je wewe hucheza Kasino Mtandaoni na umekuwa ukijiuliza ni mchezo gani rahisi na mzuri kwa ushindi? Basi Usihangaike Aviator ni rahisi zaidi kucheza na kushinda, kingine cha zaidi ni kwamba Aviator Bonanza imerudi tena Cheza zaidi ujiweke kwenye nafasi ya kushinda Samsung A23.


