Yanga Yaanza Safari Kutoka Lindi

Baada ya ushindi wa jana wa mabao 2-0 dhidi ya Namungo, klabu ya Yanga imeanza safari ya kurejea Dar es salaam kupitia Mtwara wakitokea Ruangwa ambapo jana walikuwa na kibarua kizito huko Lindi.

 

Yanga Yaanza Safari Kutoka Lindi
Yanga wameendelea kusalia kileleni baada ya jana kuchana nyavu mara mbili kupitia kwa wachezaji wao Yanick Bangala na Tuisila Kisinda ambayo yalitosha kuikandamiza Namungo huku wakiwa wamezidiwa kwa ubora.

Pointi tatu za Yanga zimewafanya wawe mbele kwa pointi nne kileleni na kuwa na matumaini ya kutetea taji lao ambalo walilichukua msimu uliopita chini ya Nasredine Nabi japokuwa kocha huyo amefungiwa michezo mitatu na faini juu.

Yanga Yaanza Safari Kutoka Lindi

Kikosi hicho kinatarajiwa kushuka dimbani kwa Mkapa siku ya Jumapili kukipiga dhidi ya Kurugenzi FC kwenye mchezo wa Azam Sports Federation Cup ambapo wao ndio mabingwa watetezi wa Kombe hilo baada ya kumtwanga Coastal Union.

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.