Sterling Kurejea Kambini Kesho

Raheem Sterling atajiunga tena na kikosi cha Uingereza cha Kombe la Dunia hapo kesho kabla ya mchezo wao wa robo fainali dhidi ya Ufaransa baada ya kumtoa Senegal katika hatua ya 16 bora.

 

Sterling Kurejea Kambini Kesho

Mshambuliaji huyo wa Chelsea alisafiri kurudi nyumbani kwake Uingereza ili kuwa na familia yake baada ya kuvamiwa katika nyumba yao na kushuhudia vitu kadhaa vya thamani vikiibiwa.

Sterling mwenye umri wa miaka 28 hakucheza katika ushindi wa Uingereza wa 3-0 katika hatua ya 16 bora dhidi mabingwa wa Afcon Senegal siku ya Jumapili, huku kocha mkuu wa Three Lions Gareth Southgate akisema Sterling anarejea nyumbani.

Uchunguzi wa polisi ulifanyika na kikosi hicho kilisema “hakukuwa na tukio la unyanyasaji na kuna vitu viligunduliwa kuibiwa.”

Sterling Kurejea Kambini Kesho

Shirikisho la Soka lilisema katika taarifa yake siku ya Alhamisi Raheem Sterling atarejea katika kambi ya Uingereza ya Kombe la Dunia huko Qatar, huku mchezaji huyo wa Chelsea akiondoka kwa muda ili kushughulikia masuala ya kifamilia lakini sasa anatarajiwa kuungana na kikosi huko Al Wakrah siku ya Ijumaa kabla ya robo fainali na Ufaransa.

Inaweza kumaanisha kurejea kwake kunakuja kuchelewa sana kwa Sterling kupata nafasi yoyote ya kuanza mchezo wa Jumamosi dhidi ya mabingwa hao watetezi, ikizingatiwa amekosa vipindi kadhaa muhimu vya mazoezi.

Sterling Kurejea Kambini Kesho

Sterling, aliyefikisha umri wa miaka 28 siku ya Alhamisi, amefunga mabao 20 katika mechi 81 za wakubwa akiwa na Three Lions. Ana bao moja hadi sasa kwenye Kombe hili la Dunia ambapo alifunga katika ushindi wa 6-2 wa ufunguzi dhidi ya Iran.

Acha ujumbe