Yanga Yapiga Chini Mpango wa Akaminko na Kipre kisa Dau Kubwa

Klabu ya Yanga inaelezwa imeachana na mpango wa kuwasajili wachezaji wawili wa klabu ya Azam James Akaminko na Kipre Junior sababu ikiwa dau kubwa.

Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya NBC walipeleka barua kwa klabu ya Azam siku kadhaa zilizopita ya kuwahitaji wachezaji hao wawili, Lakini klabu hiyo imechana na mpango huo baada ya kutajiwa kiasi kikubwa cha pesa kwa kila mchezaji na klabu ya Azam.yangaKlabu ya Azam Fc inaelezwa wamehitaji dola laki nne kwa kila mchezaji ambaye Wananchi walimuhitaji dola laki nne kwa pesa za kitanzani ni sawa ni shiilingi milioni mia tisa kwa kila mchezaji, Hivo Yanga wameamua kuachana na mpango huo baada ya kushindwa kumudu gharama hizo.

Klabu ya Yanga walihitaji wachezaji hao wawili ili kuweza kukiimarisha kikosi chao kuelekea michuano ya kimataifa msimu huu, Pamoja na kutetea mataji ambayo walitwaa msimu uliomalizika kama ubingwa wa ligi kuu na pamoja na kombe la Azam.yangaYanga pia walihitaji kuhakikisha wanaziba pengo la kiungo wao mahiri ambaye ameondoka klabuni hapo siku za hivi karibuni Feisal Salum, Na James akaminko alikua anaonekana anaweza kua mbadala sahihi wa kiungo huyo kutoka visiwani Zanzibar.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.