Winga wa klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza Jadon Sancho amefurahi kufunga bao tena ndani ya kikosi hicho baada ya kukosekana kwa zaidi ya miezi mitano ndani ya timu hiyo.
Winga Jadon Sancho amekua nje ya uwanja kwa muda mrefu akiwa anasumbuliwa na majeraha pamoja na saikolojia yake haikua vizuri kama ambavyo kocha wa klabu hiyo Erik Ten Hag aliwahi kueleza miezi kadhaa nyuma.
Winga huyo huyo amefanikiwa kufunga bao jana katika mchezo wake wa pili tangu arejee klabuni hapo baada ya kukosekana tangu mwezi Oktoba mwaka jana, Jana mchezaji huyo alifunga bao la kusawazisha baada ya klabu yake kutanguliwa kwa mabao mawili na klabu ya Leeds United katika mchezo uliomalizika kwa mabao mawili kwa mawili.
Mchezaji huyo aliandika kupitia mitandao yake ya kijamii na kusema “Siwezi kukuambia kwa namna gani nilikosa hisia kama hii, Timu imeonesha sifa nzuri kubaki kwenye mchezo, Tutaenda tena wikiendi”
Baada ya Jadon Sancho kufanya vizuri katika mchezo wa jana amemfanya kocha wa klabu hiyo kumpongeza mchezaji huyo kutokana na ubora ambao ameuonesha katika mchezo wa jana, Hiyo inaweza kumpa nguvu mchezaji na kuweza kumrejesha kwenye ubora wake ambao amekua nao tangu akiwa klabu ya Borussia Dortmund.

