Klabu ya Liverpool na Newcastle watashuka dimbani leo kumenyana katika mchezo mkali wa ligi kuu ya Uingereza utakaopigwa katika dimba la St.James Park.
Mchezo huo unatarajiwa kua mkali kwani timu zote zinaonekana zipo kwenye nafasi nzuri ya kushinda, Kwani vilabu vyote vimefanya usajili mzuri na vina wachezaji wazuri na kufanya kua moja ya mchezo mzuri wa kutazamwa sana leo.
Klabu ya Liverpool leo watakua ugenini katika mchezo dhidi ya Newcastle ambao nao wanahitaji matokeo ya ushindi baada ya kupoteza mchezo uliomalizika dhidi ya Manchester City wikiendi iliyomalizika.
Mchezo wa leo ni mgumu kwelikwlei kwani vilabu vyote vinahitaji kupata matokeo ya ushindi ili kujiweka katika mazingira mazuri, Huku majogoo wao wakijitahidi kuendelea kulinda rekodi ya kutokufungwa katika michezo yake miwili yake ya awali.
Newcastle wao watakua wanahitaji alama tatu angalau kuondoka katika jinamizi la kupoteza mchezo uliomalizika, Mchezo huu unatarajiwa kua mkali sana ambapo mpaka wakati huu rekodi zinawabeba Liverpool kwkaua ni muda mrefu hawajapoteza dhidi ya Newcastle.

