Viungo wa klabu ya Real Madrid Toni Kroos na Luca Modric wanaelezwa hawana furaha kuanzia benchi kwenye michezo ya klabu hiyo wakati wao wanaamini wanastahili kuanza.
Vyanzo vya ndani kutoka klabu ya Real Maddrid vinaeleza viungo hao wawili wakongwe Toni Kroos na Luca Modric wanaamini bado wana uwezo wa kuendelea kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
Viungo hao wakongwe wamekua hawapati nafasi ya kuanza mara kwa mara ndani ya timu hiyo msimu huu, Huku nafasi wakipewa zaidi vijana wadogo walioko ndani ya timu hiyo kama Eduardo Camavinga, Fede Valverde, Aurelien Tchouameni.
Viungo hao wakongwe ambao wameongeza mkataba wa kuitumikia klabu hiyo kwa mwaka mmoja mwingine, Hivo kwasasa ambao wamekua wakianzia nje mara kwa mara kwajili ya kuwapa nafasi vijana.
Klabu ya Real Madrid ina mpango wa kutengeneza timu ambayo itajengwa na vijana ambao wapo ndani ya klabu hiyo, Hivo Luca Modric na Toni Kroos wanatakiwa kuanzia nje kwajili ya kupisha vijana ambao wataibeba timu hiyo miaka kadhaa mbele kama wao walivyofanya miaka iliyopita.

